Mwanaanga : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.6.4) (roboti Badiliko: tr:Astronot
Mstari 96: Mstari 96:
[[th:นักบินอวกาศ]]
[[th:นักบินอวกาศ]]
[[tl:Astronota]]
[[tl:Astronota]]
[[tr:Uzay insanı]]
[[tr:Astronot]]
[[uk:Астронавт]]
[[uk:Астронавт]]
[[ur:خلانورد]]
[[ur:خلانورد]]

Pitio la 01:24, 28 Machi 2011

Mwanaanga ni mtu anayerushwa katika anga la nje lililo nje ya angahewa ya dunia. Majina mengine yaliyokuwa kawaida ni "kosmonavti" (Kirusi космонавт) kwa wanaanga Warusi na "astronauti" (Kiing. astronaut) wa wanaanga kutoka Marekani. Wachina wametumia neno "taikonauti".

Mwanaanga wa kwanza katika historia ya binadamu alikuwa Mrusi Yuri Gagarin kutoka Umoja wa Kisovyeti aliyerushwa tarehe 12 Aprili 1961 kwa chombo cha angani Vostok akizunguka dunia lote mara moja katika muda wa dakika 108.

Alifuatwa 5 Mei 1961 na Alan Shepard kutoka Marekani aliyetumia chombo cha angani cha Mercury .

Mwanamke wa kwanza angani alikuwa Mrusi Valentina Tereshkova mwaka 1963.

Wanaanga wa kwanza waliofika kwenye uso wa mwezi walikuwa Wamarekani Neil Armstrong na Buzz Aldrin tar. 20 Julai 1969.

Hadi machi 2008 jumla ya watu 477 kutoka nchi 39 walifika kwenye kimo cha kilomita 100 juu ya uso wa dunia ambacho ni kimo ambako anga la nje linaanza kulingana na maelezo ya Shirikisho la Kimataifa kwa Usafiri wa Angani (Fédération Aéronautique Internationale (FAI)).

Kati ya hawa ni 24 waliofika mbali zaidi kuliko kilomita 2,000 juu ya uso wa dunia hadi njia ya mwezi kwenye anga.

Mwanaanga aliyekaa muda mrefu angani alkuwa Mrusi Sergei Krikalyov aliyefika angani mara sita akakaa jumla ya siku 803, masaa 9 na dakika 39 kwenye anga la nje.

Picha za wanaanga

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mwanaanga kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.