Mwai Kibaki : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d kubwa ---> ndogo herufi, replaced: Watu Walio Hai → Watu walio hai using AWB
Mstari 112: Mstari 112:
[[ro:Mwai Kibaki]]
[[ro:Mwai Kibaki]]
[[ru:Кибаки, Мваи]]
[[ru:Кибаки, Мваи]]
[[rw:Mwai Kibaki]]
[[simple:Mwai Kibaki]]
[[simple:Mwai Kibaki]]
[[sl:Mwai Kibaki]]
[[sl:Mwai Kibaki]]

Pitio la 20:48, 2 Januari 2011

Mwai Kibaki
Mwai Kibaki
Mwai Kibaki
Rais wa tatu wa Kenya
Tarehe ya kuzaliwa 15 Novemba 1931
Mahali pa kuzaliwa kijiji cha Gatuyaini,
tarafa ya Othaya, wilaya ya Nyeri
Chama hadi 1991 KANU, halafu DP, 2002 NARC
Alingia ofisini 2002
Alitanguliwa na Daniel arap Moi
Dini Mkristo Mkatoliki
Elimu yake chuo kikuu cha Makerere, LSE London
Digrii anazoshika M.Sc. (Public Finance
Kazi mwalimu wa chuo, mwanasiasa


Mwai Kibaki ni rais wa tatu wa Jamhuri ya Kenya akiwa ametanguliwa na Rais wa Kwanza wa Kenya,Mzee Jomo Kenyatta, na Daniel Arap Moi. Jina lake la kubatizwa ni Emilio Stanley .

Kibaki alisoma uchumi, historia na sayansi ya siasa katika chuo kikuu cha Makerere, Kampala, Uganda. Akiwa mwanafunzi Makerere, Kibaki alikuwa ni mwenyekiti wa chama cha wanafunzi toka Kenya, Kenya Students' Association. Alipomaliza masomo yake mwaka 1955 alipewa tuzo kutokana na kufanya vyema katika mitihani. Tuzo hiyo ilimwezesha kwenda kusoma katika chuo cha London School of Economics. Alipomaliza masomo alikwenda kufundisha katika chuo kikuu cha Makerere. Baadaye aliacha kazi ya kufundisha na kuwa mtendaji mkuu wa chama cha Kenya African National Union.

Kibaki, licha ya kuwa mbunge, amewahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha, Mwenyekiti wa Tume ya Mipango, Waziri wa Biashara na Viwanda, na Waziri wa Fedha. Moi alipoingia madarakani baada ya kifo cha Jomo Kenyatta, Kibaki aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais.

Mwaka 1988 Kibaki alianza kuwa na mgongano na Rais Moi. Mwaka huo alivuliwa Umakamu wa Rais na kupelekwa Wizara ya Afya.

Mwaka 1991 Kibaki aliondoka chama cha KANU na kuanzisha chama cha Democratic Party. Katika uchaguzi wa Urais wa mwaka 1991, Kibaki alikuwa wa tatu na mwaka 1997 alikuwa wa pili.

Uchaguzi wa urais 2002

Katika uchaguzi wa 2002 Kibaki alishinda na kutangazwa kuwa Rais wa Kenya. Alikuwa mgombea wa maungano wa vikundi vingi vya upinzani vilivyoshirikiana kwa jina la "NARC".

Kibaki ameweka historia mwezi Novemba, 2005 baada ya kuwa Rais wa kwanza nchini Kenya kuondoa baraza lote la mawaziri kufuatia kura ya maoni ambayo ilikuwa inahusu katiba mpya ya Kenya. Kibaki alikuwa upande wa kundi lililokuwa likiunga mkono katiba hiyo kambi ya ndizi. Kundi lililokuwa likiipinga katiba hiyo kambi ya machungwa lilipata ushindi.

Uchaguzi wa urais 2007

Uchaguzi wa 28 Desemba 2007 ulimrudisha Kibaki kwa kipindi cha pili kama rais. Uchaguzi huu ulipingwa na chama cha upinzani,ODM , na watazamaji wa kimataifa kuwa matokeo hayo hayakuwakilisha matakwa ya Wakenya. Mpinzani wake mkuu, Raila Odinga alikuwa mbele katika hesabu za kura hadi Kamati ya Uchaguzi iliposimamisha kuhesabu; baada ya kuendelea na matanganzo Kibaki alionekana kuwa mbele. Kulikuwa na hofu ya kwamba matokeo ya majimbo ya uchaguzi kadhaa yalibadilishwa yakiegemea upande wake kwa kumwongezea kura. Hisia hizi zilisababisha ghasia kuibuka Nairobi, Kisumu, Eldoret, Kericho, Mombasa na sehemu zinginezo nchini. Kibaki aliapishwa upya kuwa rais wa Kenya masaa machache tu baada ya kutangazwa kuwa mshindi; hafla ilifanywa katika Bustani ya Ikulu ya Nairobi mbele ya waalikwa wachache walioruhusiwa kushuhudia.

Kamati iliyobuniwa tutathmini ukweli wa mambo katika uchaguzi huo wa urais, iliyoongozwa na jaji mstaafu kutoka Africa Kusini Johann Kriegler, iliripoti kwamba mshindi katika uchaguzi huo wa urais wa 2007 hangeweza kujulikana. Hii ni kwa sababu wizi wa kura ulifanyika katika sehemu nyingi nchini na ulitekelezwa kule mashinani na wafuasi wa wapinzani wote katika kinyang'anyiro cha Urais. Kriegler pia alielekeza lawama kwa Tume ya Uchaguzi ya Kenya kwa kutowajibika katika utendakazi, na ripoti hiyo ya Krieger ilipendekeza tume hiyo ivunjwe na ibadilishwe na ingine iliyo huru.

Kinyume cha uchaguzi wa rais uchaguzi wa Bunge la Kenya 2007 uliendelea bila matatizo makubwa.

Serikali ya Januari 2007

Baada ya kutangazwa kuwa rais mpya Kibaki aliteua mawaziri 17 kama awamu ya kwanza ya serikali akiacha nafasi nyingine serikalini kando kwa muda.[1]

(1) Makamu wa Rais na waziri wa mambo ya ndani: Stephen Kalonzo Musyoka
  • (2) Waziri wa utawala wa mikoa na usalama wa ndani katika Ofisi ya Rais: George Saitoti
  • (3) Waziri wa ulinzi katika Ofisi ya Rais: Yussuf Mohamed Haji
  • (4) Waziri wa mipango maalumu katika Ofisi ya Rais: Dr. Naomi Namsi Shaban
  • (5) Waziri wa utumishi wa serikali katika Ofisi ya Rais: Asman Abongotum Kamama
  • (6) Waziri wa fedha: Amos Muhinga Kimunya
  • (7) Waziri wa elimu: Sam Ongeri
  • (8) Waziri wa mambo ya nje: Moses Wetangula
  • (9) Waziri wa serikali ya mitaa: Uhuru Kenyatta
  • (10) Waziri wa habari na mawasiliano: Samuel Lesuron Poghisio
  • (11) Waziri wa maji na umwagiliaji: John Munyes
  • (12) Waziri wa nishati: Kiraitu Murungi
  • (13) Waziri wa barabara na kazi za umma : John Njoroge Michuki
  • (14) Waziri wa sayansi na teknolojia: Noah M. Wekesa
  • (15) Waziri wa sheria na mambo ya katiba: Martha Karua
  • (16) Waziri wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki: Dr. Wilfred Machage
  • (17) Waziri wa usafiri: Chirau Ali Mwakwere

Viungo vya Nje

  1. http://www.eastandard.net/news/?id=1143980114 Kibaki names cabinet EA Standard 08-01-2008