Kano (jimbo) : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
dNo edit summary
Mstari 18: Mstari 18:
[[en:Kano State]]
[[en:Kano State]]
[[fr:État de Kano]]
[[fr:État de Kano]]
[[id:Kano (negara bagian Nigeria)]]
[[ja:カノ州]]
[[ja:カノ州]]
[[nl:Kano (staat)]]
[[nl:Kano (staat)]]

Pitio la 07:42, 28 Aprili 2007

Jimbo la Kano

Kano ni jimbo la kujitawala katika kaskazini ya Nigeria. Mji mkuu ni Kano mjini.

Jimbo la Kano limepakana na majimbo ya Katsina, Jigawa, Kaduna na Bauchi. Jimbo lilianzishwa tar. 27 Mei 1967. Gavana wa kwanza alikuwa Abdu Bako kuanzia 1967 hadi Julai 1975. Ibrahim Shekarau amekuwa gavana tangu 29 Mei 2003.

Eneo la jimbo ni 20,131 km², idadi ya wakazi 10,077,638 (mwaka 2005). Msongamano wa watu hufikia wakazi 501 kwa kilimita ya mraba.

Jimbo lina maeneo ya utawala 44 ("Local Government Areas"). Haya ni: Ajingi, Albasu, Bagwai, Bebeji, Bichi, Bunkere, Dala, Dambatta, Dawakin-Kudu, Dawakin-Tofa, Doguwa, Fagge, Gabasawa, Garko, Garum-Mallam, Gaya, Gazewa, Gwale, Gwarzo, Kabo, Kano Municipal, Karaye, Kibiya, Kiru, Kumbotso, Kunchi, Kura, Madobi, Makoda, Minjibir, Nassarawa, Rano, Rimin-Gado, Rogo, Shanono, Sumaila, Takai, Tarauni, Tofa, Tsanyawa, Tudun-Wada, Ungongo, Warawa na Wudil.

Kano ni kitovu cha biashara na uzalishaji mali nchini. Asilimia ya umwagiliaji wa mashamba inazidi majimbo yote na kuruhusu kilimo mwaka wote.