Bweha : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d roboti Badiliko: ro:Șacal
d roboti Nyongeza: da:Sjakal
Mstari 59: Mstari 59:
[[ca:Xacal]]
[[ca:Xacal]]
[[cs:Šakal]]
[[cs:Šakal]]
[[da:Sjakal]]
[[de:Schakal]]
[[de:Schakal]]
[[en:Jackal]]
[[en:Jackal]]

Pitio la 13:20, 28 Juni 2010

Mbweha

Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Oda: Carnivora
Familia: Canidae
Jenasi: Canis

Mbweha kwa kimombo ‘jackal’ (kutoka kwenye neno la Kituruki çakal, kupitia neno la Kipersia ‘shaghal’ moja kwa moja kutoka Sanskrit. [1][2]. Ni mmoja wa spishi mdogo tatu (wakati mwingine nne) za familia ya Canidae, inayopatikana Afrika, Asia na kusini mwa Ulaya. [3] Mbweha hawa wana sehemu kubwa ya ikolojia sawa na coyote, (mbweha wa America). Huko Amerika ya kaskazini, ile ya wanyama wa umbo la kawida, wala mizoga na pia wanaokula mchanganyiko wa majani na nyama. Miguu yao mirefu na meno chonge yaliyopinda yamekua hivyo kwa ajili ya kuwinda mamalia wadogo, ndege na reptilian. Wayo mkubwa na mifupa ya miguu iliyounganika inawapa wao uwezo wa kukimbia umbali mrefu, na kuweza kuhilimili mpaka mwendo kasi kilometa 16 kwa saa kwa umbali mrefu. Huwa na nguvu sana (na waliochanganyika) wakati wa mashariki na alfajiri.

Katika jumuiya ya mbweha ujamaa ni ule wa mwenzi wa mmoja mmoja, ambao wawili hao hulinda himaya yao dhidi ya mbweha wengine. Himaya hizi hulindwa, mara nyingi kwa kuwafukuza na kuweka alama kuzunguka himaya yao kwa kutumia mkojo na kinyesi. Himaya hiyo inaweza kuwa kubwa kiasi cha kuchukua watoto mpaka watakapo kuwa wakubwa na kuweza kuanzisha himaya zao wenyewe. Mbweha mara kadhaa huweza kujikusanya kwenye makundi madogomadogo, kwa mfano wakati wa kuokota mizoga, lakini mara nyingi huwinda mmoja mmoja au kama jozi.

Uanishaji na mahusiano

Mnamo mwaka 1816, kwenye juzuu ya tatu ya Lorenz Oken isemayo 'Lehrbuch der Naturgeschichte’ , mwandishi alipata uwiano na mfanano kubwa wa mpangilio wa meno kwa mbweha na wale mbweha wa Amerika ya kaskazini, coyotes’ na kuwaweka kwenye spishi moja lakini jenasi tofauti ‘Thos.’ kwa ujumla maelezo yote yaliotumika kuelezea mgawanyo wa jenasi yalikuwa ya kuhusisha tu bila ya kuwa na kumbukumbu na vipimo sahihi kuzingatia tofauti baina ya spishi ambazo zinaweza kuzingatiwa. Angel cabreva, katika kitabu chake cha 1932 kuhusu wanyama wa Morocco, kwa ufupi aligusia kuhusu swali juu ya kuwepo kwa “cingulum” kwenye maggso ya juu ya mbweha, na kutokuwepo kwa wanafamilia wengine wa Canis kuna dhibitisha mgawanyo wa jenasi na Canabia,. Hatimaye alichagua jenus ambayo haigawanyiki na kuiita kwa mbweha kama ‘Canis’

Nadharia ya Oken ilikuwa na mchango mdogo kwenye upaji wa majina ya uanishaji; ingawa ilifufuliwa tena mnamo 1914 na Edmund Heller aliyechukua nadharia ya jenasi mpya. Majina ya Heller aliyotoa kwa aina ya spishi kadhaa za mbweha na spishi zake ndogo bado yanatumika japo jenasi yamebadilika kutoka Thos mpaka Canis [4] Tafiti za kisasa zimeonesha mahusiano baina ya spishi za mbweha mbali na kufanana kwao muonekano wanje, wote hawahusiani kwa ukaribu. Mbweha mwenye mistari mgongoni na wale wenye mgongo mweusi wanakaribiana sana lakini wanatofautiana sana na mbwa mwitu mya, hasa kutoka Afrika na Eurasia. Mbweha dhahabu na mbwa mwitu wa Ethiopia ni sehemu ya umuhimu na pia hujumuisha mbwa mwitu wa kijivu, mbwa hufunzwa na mbweha wa Amerika. [5]. Wanapo zalishwa kwa mchanganyiko mbwa na mbweha hutoa watoto wenye matatizo ya uzazi, magonjwa ya mawasiliano.

Spishi;

Golden jackal (Canis aureus)
Side-striped jackal (Canis adustus)
Black-backed jackal (Canis mesomelas)
Ethiopian wolf (Canis simensis) – wakati mwingine hufahamika kama mbweha mwekundu au Simian jackal, lakini kwa kiasi kikubwa hufahamika mkama mbwa mwitu

Matumizi ya kale

Mungu wa kale wa Misri, na wa chini diniani, Anubis, na mwenye kuzuia maiti isioze, Anubis alioneshwa kama mwanume mwenye kichwa cha mbweha. Leo ni wanyama wanaoonekana sana kwenye safari na kuonekana sana nje ya mbuga za wanyama, pia na kuonekana sana kwenye maeneo karibu na makazi ya watu.

Matumizi ya msimu

[[6]] Mbweha wa dhahabu “golden jackal”

Taswira maarufu, japo si sahihi sana ya mbweha kama wala mizoga kwa kiasi fulani imepelekea tafsiri mbaya. • Msemo”umbweha” wakati fulani hutumuka kuelezea kazi ifanywayo na mfanyakazi wa chini kwaajili ya kuokoa mda kwaajili ya mtu mkubwa (kwa mfano- mwanasheria mdogo anaweza kufanya kazi nyingi kwa niabaa ya wakili). Hii imetokana na ule utamaduni wa kwamba mbweha kumuongoza simba kwenye mawindo yake. Neno hili mli wakati mwingine hutumika kuelezea tabia ya mtu anaye penda kujaribu kutumia na kufaidi mizoga ya mtu aliyepatwa na janga fulani. Mfano: kuvamia na kuiba kwenye kijiji kilicho kubwa na mafuriko na wakazi wake wamekimbia.

[[7]] Pundamilia na mbweha huko Ngorongoro Crater, Tanzania