Data : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d roboti Nyongeza: ur:معطیات
d roboti Nyongeza: is:Gögn
Mstari 144: Mstari 144:
[[hu:Adat]]
[[hu:Adat]]
[[id:Data]]
[[id:Data]]
[[is:Gögn]]
[[it:Dato]]
[[it:Dato]]
[[ja:データ]]
[[ja:データ]]

Pitio la 18:20, 27 Desemba 2009

Data inamaanisha makundi ya habari ambayo inawakilisha sifa qualitative au quantitative za variable au seti ya variables. Data (wingi wa jina "Datum", ambayo kutumika nadra) kwa kawaida ni matokeo ya vipimo na inaweza kuwa msingi wa graph, picha, au uchunguzi wa seti ya variables. Mara nyingi Data huchukuliwa kama kiwango cha chini kabisa kwa ujumla ambapo habari na maarifa yaweza kutolewa


Asili ya Jina

Neno data ni wingi wa neno la Kilatini, Datum, ambayo inamaanisha "kutoa", kwa hivyo inaweza kumaanisha "kitu kutolewa". Participle ya "kutoa" imetumiwa kwa muda wa milenia, kama taarifa iliyokubaliwa katika fn, Data. Katika mijadala ya matatizo katika geometri, hisabati, uhandisi, na kadhalika,maneno givens na data hutumika yakibadilishana.Pia, data huwakilisha fact, takwimu, na wazo. Matumizi kama haya ndiyo asili ya data kama dhana katika sayansi ya tarakilishi au kompyuta ukipenda: data ni idadi, maneno, picha, nk, haya yote yanakubaliwa kama data.


Matumizi ya Kiingereza

Katika Kiingereza, neno Datum bado linatumika kwa ujumla kama "kupewa kitu". Katika masomo ya kutengeneza ramani Jiografia, ‘nuclear magnetic resonance’ na kuchora kiufundi mara nyingi hutumika kurejea datum moja maalum ambalo umbali wa data nyinginezo hupimwa. Kipimo chochote au matokeo yoyote ni Datum, lakini data point hujulikana sana, ingawa hujirudiarudia. Datum zote mbili (angalia matumizi katika makala ya Datum) na wingi wa neno la kiasili la Kilatini, data, hutumika kama wingi wa neno Datum katika Kiingereza, lakini data kwa kawaida hutumika kama jina la umoja na hutumika pamoja na kitenzi katika fomu ya umoja, hasa katika matumizi ya siku baada ya siku. Kwa mfano, Hii ni data yote kutoka kwa majaribio . Utumizi huu ni si thabiti kutokana na kanuni za sarufi za Kilatini na mila ya Kiingereza (Haya yote ni data kutoka katika majaribio).


Baadhi ya mifumo ya Uingereza na ya kimataifa ya kielimu, kisayansi na kitaalamu [8] zinahitaji kwamba waandishi watumie data kama wingi wa jina. Mashirika mengine ya kimataifa, kama vile IEEE Computer Society, huruhusu utumizi wake kama jina la umoja au wingi, msingi wake ukiwa mapendeleo ya mwandishi. Air Force Flight Test Center upande wake, husema kuwa neno data daima lipo katika hali ya wingi, kamwe haipo katika hali ya umoja.


Data kwa sasa mara nyingi hutumiwa kama jina la umoja katika matumizi rasmi, lakini matumizi katika machapisho ya kisayansi yaonyesha mgawanyiko kati ya Marekani na Uingereza. Marekani, neno data wakati mwingine hutumika katika umoja, ingawa wanasayansi na waandishi wa sayansi mara nyingi hutumia neno hilo kama wingi kama ilivyotumiwa jadi. Baadhi ya magazeti makubwa kama vile New York Times hutumia neno hilo katika hali ya umoja au wingi. Katika New York Times ya misemo "data za utafiti bado zinachambuliwa" na "mwaka wa kwanza ambao data inapatikana" imeonekana siku hiyo hiyo. Katika sayansi ya kuandika data mara nyingi hutumika kama wingi, kama kwamba data hizi hazisaidi wakati wakuhitimisha, lakini watu wengi sasa hufikiria data kuwa katika hali umoja kama taarifa na hutumia hali ya umoja kwa ujumla angalau katika matumizi ambao si ya kisayansi. Matumizi ya Uingereza sasa inakubali sana utumizi wa neno data katika hali ya umoja katika kiwango cha Kiingereza, zikiwemo utumizi wa kila siku wa magazeti angalau katika matumizi yasiyo ya kisayansi. Uchapishaji wa kisayansi wa Uingereza bado hutumia neno data katika hali ya wingi. Baadhi ya mifumo ya vyuo vikuu vya Uingereza vinapendekeza utumizi wa neno data katika hali ya umoja na wingi na baadhi hupendekeza utumizi wake katika hali ya umoja likihusishwa na kompyuta au tarakilishi.


Raw data kwa lugha ya kimombo ni mkusanyiko wa idadi, picha au matokeo mengine kutoka kwa vifaa ili kuvibadilisha kuwa ishara, ambazo bado hazijasindikwa. Data hizo kwa kawaida hupitia usindikaji zaidi kwa binadamu au huingizwa katika kompyuta, huhifadhiwa na hupitia usindikaji huko, au hupelekwa (matokeo) kwa binadamu mwingine au kompyuta nyingine (kutumia waya). Raw data ni jina ambalo hubadilika; usindikaji wa data kwa kawaida hutokea hatua kwa hatua, na "data iliyosindikwa" kutoka hatua moja inaweza kuonekana kama "data ambayo haijasindikwa"(raw data) katika hatua ijayo.


Vifaa vya tarakilishi vya muwasho vimewekwa katika vikundi kulingana na njia ambazo zinawakilisha data. Tarakilishi ya aina ya "Analog" inawakilisha Datum kama umbali or pozishoni. Tarakilishi ya aina ya "Digital" inawakilisha Datum kama mlolongo wa ishara inayotolewa kutoka alfabeti isiyobadiliki. Tarakilishi za aina ya "Digital" zinazotumika sanasana hutumia alfabeti ya "binary", ambazo kwa kawaida ni idadi "0" na "1". Aina tofauti za uwakilishaji zinazojulikana sana , kama vile idadi au alfabeti, vinajengwa kutoka kwa alfabeti ya "binary".


Baadhi ya fomu maalum ya data huwa ni tofauti. Programu ya kompyuta ni mkusanyijo wa data, ambayo inaweza kufasiriwa kama maelekezo. Baadhi ya lugha za kompyuta hubainisha kati ya program ya kompyuta na data nyinginezo ambazo huendesha programu za kompyuta, lakini katika baadhi ya lugha za kompyuta, hasa Lisp na lugha zinazofanana, programu haziwezi kutofautishwa kimsingi kutoka data nyinginezo. Ni muhimu pia kutofautisha metadata, ambayo ni maelezo ya data nyinginezo. Jina lenye maana sawa na metadata lakini la kitambo ni "ancillary data". Mfano wa metadata ni maktaba ya katalogi, ambayo ni maelezo ya yaliyomo vitabuni.


Data ya majaribio inahusu data iliyotengenezwa katika muktadha wa uchunguzi wa kisayansi kupitia kutazama au kuchunguza na kurekodi.


Maana ya data, taarifa na maarifa

Maneno taarifa na maarifa mara nyingi hutumika katika dhana zinazobadilika. Tofauti kuu ni katika kiwango cha ujumla inayozingatiwa. Data iko katika ngazi ya chini, taarifa ni ngazi ya pili, na hatimaye, maarifa ni ngazi ya juu kati ya zote tatu. Data, kibinafsi haina maana yoyote. Ili data ibadilishwa kuwa taarifa, ni lazima data ifasiriwe na kupatiwa maana. Kwa mfano, urefu wa Mlima Everest kwa ujumla inachukuliwa kama "data", kitabu kuhusu sifa za Mlima Everest zinaweza kuonekana kama “taarifa” na ripoti yenye taarifa kuhusu njia bora ya kufikia kilele cha Mlima Everest inaweza kuchukuliwa kama "maarifa".


Taarifa kama dhana huleta maana tofauti, kutoka kwa matumizi ya kila siku hadi mipangilio za kiufundi. Tukizungumza kwa ujumla, dhana ya taarifa inahusiana kwa karibu na wazo za vikwazo, mawasiliano, kudhibiti, data, umbo, mafundisho, maarifa, maana, kichocheo cha kiakili, muundo, mtazamo, na uwakilishi.


Beynon-Davies hutumia dhana ya ishara kutofautisha kati ya data na taarifa; data ni ishara ilhali taarifa hutokea wakati ishara zinatumiwa kumaanisha kitu fulani. [1] [2]


Ni watu na kompyuta ambao hukusanya data na kulazimisha ruwaza kwa data. Ruwaza hizi ni huonekana kama taarifa ambayo inaweza kutumika kuongeza maarifa. Ruwaza hizi zinaweza kufasiriwa kama ukweli, na zina mamlaka kama estetiska na vigezo vya kimaadili. Matukio ambayo huacha nyuma mabaki yanaweza kufikiwa data. Alama hazifikiriwi tena kama data mara tu kiungo kinachounganisha alama na mtazamo kinavunjwa. Hii inamaanisha kuwa, wakati tukio linawacha alama za khabari, alama hizo zinapata hadhi ya data. [3]


Angalia Pia

Simple English Wiktionary
Simple English Wiktionary
Wikamusi ya Kiswahili ina maelezo na tafsiri ya maana ya neno:
  • Data ya kibiologia
  • Ununuzi wa data
  • Uchambuzi wa data
  • Waya ya data
  • Data domain
  • Data element
  • Data Farming
  • Utawala wa data
  • Uadilifu wa data
  • Matengenezo ya data
  • Usimamizi wa data
  • Data mining
  • Data Modeling
  • Usindikaji wa data ya kompyuta
  • Ahueni wa data
  • Data remanence
  • Seti ya Data
  • Data warehouse
  • Database
  • Datasheet
  • Environmental data rescue
  • Metadata
  • Scientific data archiving
  • Takwimu
  • Datastructur


Marejeo

  1. P. Beynon-Davies (2002). Information Systems: An introduction to informatics in organisations. Basingstoke, UK: Palgrave. ISBN 0-333-96390-3. 
  2. P. Beynon-Davies (2009). Business information systems. Basingstoke, UK: Palgrave. ISBN 978-0-230-20368-6. 
  3. Sharon Daniel. The Database: An Aesthetics of Dignity. 


Viungo vya nje


Kigezo:FOLDOC