Mtaguso wa kwanza wa Konstantinopoli : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Mstari 35: Mstari 35:
[[la:Concilium Constantinopolitanum Primum]]
[[la:Concilium Constantinopolitanum Primum]]
[[lt:Konstantinopolio I susirinkimas]]
[[lt:Konstantinopolio I susirinkimas]]
[[mk:Втор вселенски собор]]
[[nl:Concilie van Constantinopel I]]
[[nl:Concilie van Constantinopel I]]
[[no:Første konsil i Konstantinopel]]
[[no:Første konsil i Konstantinopel]]

Pitio la 13:56, 26 Septemba 2009

Mchoro wa mtaguso wa kwanza wa Konstantinopoli.

Mtaguso wa kwanza wa Konstantinopoli ndio wa pili katika orodha ya mitaguso ya kiekumene ya Kanisa wakati wa mababu. Uliitishwa na kaisari Teodosius I ukafanyika Konstantinopoli mwaka 381.

Maaskofu 150 waliohudhuria walilaani aina mbalimbali za uzushi, hasa ule wa Masedoni wa Konstantinopoli aliyekanusha umungu wa Roho Mtakatifu, na kuthibitisha maamuzi ya mtaguso mkuu wa kwanza (Mtaguso wa kwanza wa Nisea), uliofanyika mwaka 325.

Hivyo walikiri kwamba Roho Mtakatifu pia, kama vile Yesu Mwana wa Mungu, anachanga hali ileile ya Baba.

Pamoja na hayo, walikamilisha kanuni ya imani ya Nisea ambayo kwa sababu hiyo inaitwa sasa kanuni ya imani ya Nisea-Konstantinopoli na ambayo inatumika sana hata leo katika madhehebu mbalimbali ya Ukristo, hasa katika liturujia.

Viungo vya nje