Fonolojia : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d roboti Nyongeza: sh:Fonologija
d roboti Badiliko: ar:صواتة
Mstari 14: Mstari 14:
[[Category:Isimu]]
[[Category:Isimu]]


[[ar:فونولوجيا]]
[[ar:صواتة]]
[[ast:Fonoloxía]]
[[ast:Fonoloxía]]
[[be:Фаналогія]]
[[be:Фаналогія]]

Pitio la 00:48, 14 Juni 2009

Fonolojia ni tawi la sayansi ya isimu. Inashughulikia uchunguzi wa mfumo wa sauti katika lugha fulani, kwa mfano ugawanyaji wa irabu na konsonanti. Matokeo ya uchunguzi wa kifonolojia yana umuhimu katika kubuni alfabeti. Dhana ya fonolojia inajipambanua vizuri zaidi ikifasiliwa kwa kutofautishwa na fonetiki. Wakati fonetiki ni taaluma inayochunguza sauti zitamkwazo na binadamu bila kuzihusisha na lugha yoyote, fonolojia huchunguza mfumo wa sauti wa lugha mahususi kama vile sauti za Kiswahili, Kiingereza, Kimwera, na Kinyaturu. ZINGATIA: Fonetiki huchunguza sauti zote zitamkwazo na binadamu; fonolojia huchunguza MFUMO WA SAUTI wa lugha mahususi.

Hivyo, fonetiki huchunguza sauti nyingi kadri iwezekanavyo, lakini fonolojia huchunguza sauti chache tu zilizomo katika mfumo wa sauti wa lugha husika. Mathalani, mfumo wa sauti wa lugha ya Kiswahili una sauti thelathini tu (irabu tano na konsonanti ishirini na tano).

Jambo lingine la kuzingatia ni vipashio vya kiuchambuzi vya matawi haya mawili. Wakati fonetiki kipashio chake cha msingi ni FONI, fonolojia kipashio chake cha msingi ni FONIMU. Kwa kuzingatia maelezo ya hapo awali, ni wazi kuwa FONI ni nyingi zaidi kuliko FONIMU, kwakuwa FONI ni kila sauti itamkwayo na binadamu, wakati FONIMU ni sauti zile tu zilizomo katika mfumo wa sauti wa lugha mahususi. Hivyo, kuna FONIMU za Kiswahili, za Kiingereza, za Kichina, n.k., lakini FONI si za lugha yoyote na wala uwezi sema kwa uhakika kuna FONI ngapi, kwakuwa bado kuna lugha nyingi duniani ambazo bado hazijatafitiwa.

Mchangiaji: achipila@yahoo.co.uk, 11:22, 19 Sept. 2008.

Marejeo

  • TUKI 1990, "Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
  • Massamba, David 2004, "Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam