Isa : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
 
No edit summary
Mstari 11: Mstari 11:
'''Ujumbe wake'''
'''Ujumbe wake'''


Nabii Isa (AS) aliletwa kwa wanadamu kufikisha ujumbe kwao wa kuwafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja hana mwenzake, na kuwa Yeye pekee ndiye mwenye kustahiki kuabudiwa kwa haki, na ujumbe huu ndio ujumbe uliotumwa kwa Mitume na Manabii wote kwa wanadamu, naye alikuja kutilia mkazo na kusisitiza jambo hili na kupa nguvu tume za Mitume na Manabii waliopita. Ujumbe wake ulikuwa ni wa mwisho kabla ujumbe wa Mtume Muhammad (SAW) ambao ndio ulikuwa wa mwisho kabisa kwa wanadamu wote.
Nabii Isa (AS) aliletwa kwa wanadamu kufikisha ujumbe kwao wa kuwafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja hana mwenzake, na kuwa Yeye pekee ndiye mwenye kustahiki kuabudiwa kwa haki, na ujumbe huu ndio ujumbe uliotumwa kwa Mitume na Manabii wote kwa wanadamu, naye alikuja kutilia mkazo na kusisitiza jambo hili na kupa nguvu tume za Mitume na Manabii waliopita. Ujumbe wake ulikuwa ni wa mwisho kabla ya ujumbe wa Mtume Muhammad (SAW) ambao ndio ulikuwa wa mwisho kabisa kwa wanadamu wote.

'''Itikadi ya Kikristo kuhusu Isa (AS)'''

Wakristo au Manasara wanahitalifiana katika itikadi yao kuhusu Nabii Isa (AS), kwani kuna wanaomchukulia kuwa ni mtoto wa Mungu, na wengine wanaomuitakidi kuwa ni Mungu, na kuna kundi linalomchukulia kuwa ni Mtume au Nabii. Makundi haya yalitafautiana baada ya kuondoka Nabii Isa (AS) ulimwenguni na kuwawacha wafuasi wake waendeleze kazi yake ya kutangaza dini ya Mwenyezi Mungu. Wafuasi waliokuja baada yake, mbali na wale kumi na mbili waliokuwa pamoja naye, walikuja na fikra na mawazo mengine kuhusu Isa au Yesu kama anavyojulikana na Wakristo, na baada ya muda waligawanyika makundi mbali mbali, wakiwa wengine wanamuamini kuwa ni Mtume na Nabii kama alivyowafundisha na wengine wakawa wanamuamini kama ni mtoto wa Mungu au Mungu kwa sababu ya miujiza mengi aliyokuja nayo.

Miujiza ya Nabii Isa (AS):

Nabii Isa (AS) au Yesu alipewa na Mwenyezi Mungu miujiza mbali mbali kumsaidia katika kazi yake ya kutangaza dini ya Mwenyezi Mungu, kwani ilikuwa ni kawaida kwa Mtume au Nabii kuonyesha miujiza kwa watu au kaumu yake ili awathibitishie kuwa yeye kweli ni mjumbe aliyeletwa na Mola wa ulimwengu huu. Mitume waliotangulia kabla ya Nabii Isa, kama Nuh na Ibrahim na Musa na wengineo wote walikuja na miujiza mbali mbali


Salim Elhaj
Salim Elhaj

Pitio la 12:05, 27 Machi 2005

Nabii Isa (AS)

Nabii Isa (AS) ni Mtume anayeaminiwa na Waislamu kama mmojawapo wa Mitume mitukufu wa Mwenyezi Mungu walioletwa kwa ajili ya kuwaongoza wanadamu duniani, naye ni miongoni mwa Mitume wakubwa ambao Mwenyezi Mungu amewasifu kwa subira yao na ustahmilivu wao mkubwa. Nao ni Manabii Nuhu na Ibrahim na Musa na Isa na Muhammad (amani na rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao).

Nabii Isa (AS) ni mmojawapo wa 124,000 wa mfululizo wa Mitume na Manabii wa Mwenyezi walioletwa ulimwenguni kuwaletea ujumbe wanadamu wa Mwenyezi Mungu kuhusu upweke na umoja wake, na kumuabudu Yeye peke yake akiwa ndiye Muumba na Mruzuku wao hapa duniani. Watume na Manabii hawa wameletwa katika zama mbali mbali na kwa watu, kaumu na umma mbali mbali, na mfululizo huu ulianza na Adam (AS) baba wa wanadamu wote hadi Mtume Muhammad (SAW) akiwa ndiye wa mwisho katika Manabii na Mitume.

Kuzaliwa kwake

Nabii Isa (AS) alizaliwa na bibi Maryam kimiujiza, kwani alizaliwa bila ya baba kwa amri ya Mola wake ambaye alimletea Jibrili (AS) kumtangazia kupata kwa mtoto mtukufu. Baada ya kuzaliwa, Nabii Isa (AS), alisema utotoni mwake akiwa bado mchanga, ukiwa ni muujiza mwengine kwa watu ili kuwaonyesha kuwa yeye si mtoto wa kawaida, na kuwa mamake hana dhambi ya kuja kwake bila ya baba.

Ujumbe wake

Nabii Isa (AS) aliletwa kwa wanadamu kufikisha ujumbe kwao wa kuwafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja hana mwenzake, na kuwa Yeye pekee ndiye mwenye kustahiki kuabudiwa kwa haki, na ujumbe huu ndio ujumbe uliotumwa kwa Mitume na Manabii wote kwa wanadamu, naye alikuja kutilia mkazo na kusisitiza jambo hili na kupa nguvu tume za Mitume na Manabii waliopita. Ujumbe wake ulikuwa ni wa mwisho kabla ya ujumbe wa Mtume Muhammad (SAW) ambao ndio ulikuwa wa mwisho kabisa kwa wanadamu wote.

Itikadi ya Kikristo kuhusu Isa (AS)

Wakristo au Manasara wanahitalifiana katika itikadi yao kuhusu Nabii Isa (AS), kwani kuna wanaomchukulia kuwa ni mtoto wa Mungu, na wengine wanaomuitakidi kuwa ni Mungu, na kuna kundi linalomchukulia kuwa ni Mtume au Nabii. Makundi haya yalitafautiana baada ya kuondoka Nabii Isa (AS) ulimwenguni na kuwawacha wafuasi wake waendeleze kazi yake ya kutangaza dini ya Mwenyezi Mungu. Wafuasi waliokuja baada yake, mbali na wale kumi na mbili waliokuwa pamoja naye, walikuja na fikra na mawazo mengine kuhusu Isa au Yesu kama anavyojulikana na Wakristo, na baada ya muda waligawanyika makundi mbali mbali, wakiwa wengine wanamuamini kuwa ni Mtume na Nabii kama alivyowafundisha na wengine wakawa wanamuamini kama ni mtoto wa Mungu au Mungu kwa sababu ya miujiza mengi aliyokuja nayo.

Miujiza ya Nabii Isa (AS):

Nabii Isa (AS) au Yesu alipewa na Mwenyezi Mungu miujiza mbali mbali kumsaidia katika kazi yake ya kutangaza dini ya Mwenyezi Mungu, kwani ilikuwa ni kawaida kwa Mtume au Nabii kuonyesha miujiza kwa watu au kaumu yake ili awathibitishie kuwa yeye kweli ni mjumbe aliyeletwa na Mola wa ulimwengu huu. Mitume waliotangulia kabla ya Nabii Isa, kama Nuh na Ibrahim na Musa na wengineo wote walikuja na miujiza mbali mbali

Salim Elhaj