Songea (mji) : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d roboti Nyongeza: tr:Songea
d roboti Nyongeza: sv:Songea
Mstari 27: Mstari 27:
[[pl:Songea]]
[[pl:Songea]]
[[ro:Songea]]
[[ro:Songea]]
[[sv:Songea]]
[[tr:Songea]]
[[tr:Songea]]

Pitio la 02:35, 2 Desemba 2008

Songea ni mji nchini Tanzania ambao ni makao makuu ya Mkoa wa Ruvuma. Kulingana na sensa ya mwaka 2002 idadi ya wakazi wake ilihesabiwa kuwa 131,336 [1].

Kuna barabara ya lami kutoka Songea kupitia Njombe hadi barabara kuu ya Dar es Salaam - Mbeya. Barabara ya kwenda pwani kupitia Tunduru na Masasi ni mbaya mara nyingi haipitiki wakati wa mvua.

Jiografia

Mji uko kwenye kimo cha m 1210 juu ya UB katika nchi ya Ungoni kwenye nyanda za juu za kusini za Tanzania. Chanzo cha mto Ruvuma kipo karibu na mji.

Historia

Jina la Songea ni kumbukumbu ya chifu Songea wa Wangoni aliyekuwa na ikulu yake hapa wakati wa kuenea kwa ukoloni wa Ujerumani akauawa na Wajerumani wa kati wa vita ya majimaji.

Mji wa Songea (iliyoandikwa Ssongea wakati ule) ulianzishwa mwaka 1897 kama kituo cha kijeshi cha Kijerumani. Ukakua kuwa makao makuu ya utawala wa mkoa Songea wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.

Mazingira ya mji yaliathiriwa vibaya na vita ya majimaji na ukandamizaji wake na Wajerumani.

Songea ikaendelea kuwa makao makuu ya mkoa wakati wa uatwala wa Uingereza katika Tanganyika na baada ya uhuru katika Tanzania huria.