Maisha : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d Masahihisho aliyefanya Hasheem17 (Majadiliano) yalirejeshwa hadi sahihisho la mwisho na Riccardo Riccioni
Tag: Rollback
No edit summary
Tags: Reverted Mobile edit Mobile web edit
Mstari 24: Mstari 24:
* [http://www.ontology.co/existence.htm The Concept of Existence: History and Definitions from Leading Philosophers]
* [http://www.ontology.co/existence.htm The Concept of Existence: History and Definitions from Leading Philosophers]
* [http://www.wdl.org/en/item/2983 "A Treatise on Book Titles"] is a work by [[Sayf al-Din al-Amidi]], in Arabic, about "original" and "mental existence". It dates from 1805.
* [http://www.wdl.org/en/item/2983 "A Treatise on Book Titles"] is a work by [[Sayf al-Din al-Amidi]], in Arabic, about "original" and "mental existence". It dates from 1805.
Maisha ni pumzi + mwili yaani mafsi hai


{{mbegu}}
{{mbegu}}

Pitio la 09:30, 6 Mei 2021

Maisha ni muda ambao kiumbe hai anajaliwa kuishi. Ni hali tofauti kabisa na uzima wa milele, kwa kuwa uhai wake una mwanzo na mwisho.

Hasa mwisho unasababisha maswali: kama kila chenye mwanzo kina mwisho, ya nini kuwepo kwake? Kukosa lengo, kuwepo bure, kutokuwa na maana kunamfanya mtu ajisikie mnyonge, pengine akate tamaa ya kuishi, la sivyo ajitose kufurahia mazuri yanayopatikana maishani, lakini bila uwezo wa kuondoa moyoni ule utupu wa maana unaomtia huzuni ya dhati.

Ndiyo sababu maana ya maisha ni mojawapo kati ya masuala makuu ya binadamu duniani: hawezi kukwepa maswali ya kutoka moyoni mwake kuhusu thamani, madhumuni na umuhimu wa maisha yake.

Suala hilo linaweza kujitokeza kwake katika maswali mengi tofauti yanayohusiana, kama vile: "mbona tumekuwepo?"; "maisha yanahusu nini?" na "nini maana ya hayo yote? Binadamu anajiuliza maswali kama hayo hasa anapokabiliana na kifo, kwa mfano msiba wa ndugu au rafiki.

Hilo limekuwa suala kuu la udadisi wa sayansi, falsafa na dini tangu zamani. Hivyo kumekuwa na idadi kubwa ya majibu kutoka asili mbalimbali kadiri ya itikadi na utamaduni.

Marejeo

Viungo vya nje

Maisha ni pumzi + mwili yaani mafsi hai