Khorezmia : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Legobot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 43 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q182647 (translate me)
No edit summary
Mstari 9: Mstari 9:


[[Jamii:Asia ya Kati| ]]
[[Jamii:Asia ya Kati| ]]
[[Jamii:Nchi ya Kihistoria ya Asia]]
[[Jamii:Nchi za Kihistoria za Asia]]
[[Jamii:Jiografia ya Uzbekistan]]
[[Jamii:Jiografia ya Uzbekistan]]
[[Jamii:Jiografia ya Turkmenistan]]
[[Jamii:Jiografia ya Turkmenistan]]

Pitio la 14:39, 21 Aprili 2021

Eneo la Khorezmia leo

Khorezmia (pia: Chorasmia) ni eneo la kihistoria upande wa kusini wa Ziwa Aral. Kiini chake ni oasisi kubwa kwenye delta ya mto Amu Darya unapoingia Ziwa Aral. Upande wa mashariki kuna jangwa la Kyzylkum na upande wa magharibi nyanda za juu za Ustyurt. Leo hii eneo limegawiwa kati ya nchi za Uzbekistan, Kazakhstan na Turkmenistan.

Katika historia tangu karne ya sita KK Khorezmia ilikuwa kitovu wa falme mbalimbali. Ni pamoja pa mahali panapotajwa kama sehemu ambako dini ya Uzoroasta ilianzishwa. Msingi wa nguvu yake ilikuwa maji ya mto katika mazingira ya jangwa, rutba ya ardhi na kilimo cha umwagiliaji. Wakazi wakle walikuwa watu wenye lugha karibu na Kiajemi lakini tangu zama za Kati makabila ya kituruki yaliingia hapa hadi Kiajemi kilipotea.

Tangu mfalme Koreshi Mkuu ilitawaliwa kama jimbo la Uajemi lakini iliweza kurudisha uhuru wake. Tangu uvamizi wa Waarabu mwaka 712 ilikuwa chini ya utawala wa Kiislamu na polepole watu wake walikuwa Waislamu. Uvamizi wa Wamongolia ulileta uharibifu mwingi.

Tangu karne ya 16 Khorezmia ilipata tena kitovu cha kisiasa katika Dola la Khiva lililoendelea hadi mwaka 1920 ilipoingizwa katika Umoja wa Kisovyeti.