Rahabu : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Legobot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 17 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q1135632 (translate me)
Rescuing 1 sources and tagging 0 as dead.) #IABot (v2.0.8
Mstari 10: Mstari 10:


==Viungo vya nje==
==Viungo vya nje==
* [http://www.askmoses.com/article.html?h=254&o=2114844 Rahab] at Ask Moses .com
* [http://www.askmoses.com/article.html?h=254&o=2114844 Rahab] {{Wayback|url=http://www.askmoses.com/article.html?h=254&o=2114844 |date=20071114214519 }} at Ask Moses .com
* [http://www.debed.com/Bible/comments/rahab-the-harlot.html questions] about Rahab's actual profession.
* [http://www.debed.com/Bible/comments/rahab-the-harlot.html questions] about Rahab's actual profession.



Pitio la 17:26, 24 Januari 2021

Mchoro wa James Tissot, Kahaba wa Yeriko na Wapelelezi Wawili.

Rahabu (kwa Kiebrania רָחָב Raẖav au Rāḥāḇ, maana yake "mpana") alikuwa mwanamke wa Yeriko wakati ambapo Waisraeli, wakiongozwa na Yoshua, walivamia nchi ya Kanaani katika karne ya 13 KK.

Kitabu cha Yoshua (2:1-7) kinasimulia jinsi huyo kahaba alivyokaribisha wapelelezi wawili wa Israeli, alivyowaficha wasikamatwe na wenyeji, na alivyowadai wamuapie watamuokoa pamoja na familia yake Mungu atakawapowajalia kuteka mji huo.

Ingawa Rahabu alifanya kazi haramu akasaliti mji wake, anasifiwa na Barua kwa Waebrania (11:31) kwa imani yake iliyomuokoa na kumuingiza katika taifa la Mungu. Pia anasifiwa na Barua ya Yakobo (2:25) kama kielelezo cha mtu anayetenda mema.

Rahabu (kwa Kigiriki Ῥαχάβ, Rakhab) anatajwa na Injili ya Mathayo (1:5) katika kitabu cha ukoo cha Yesu.

Viungo vya nje