Polandi : Tofauti kati ya masahihisho
No edit summary Tags: Mobile edit Mobile web edit |
No edit summary |
||
Mstari 146: | Mstari 146: | ||
[[Jamii:Nchi za Ulaya]] |
[[Jamii:Nchi za Ulaya]] |
||
[[Jamii:Nchi za Umoja wa Ulaya]] |
[[Jamii:Nchi za Umoja wa Ulaya]] |
||
[[Jamii:Mkataba wa Schengen]] |
Pitio la 17:10, 13 Desemba 2020
Polandi |
---|
Poland (kwa Kipoland: Polska) ni nchi ya Ulaya ya Kati. Imepakana na Ujerumani upande wa magharibi, Ucheki na Slovakia upande wa kusini, Ukraine na Belarus upande wa mashariki na Bahari ya Baltiki, Lituanya na Urusi (mkoa wa Kaliningrad Oblast) upande wa kaskazini.
Jiografia
Ardhi ya Poland ni tupu tu kufikia kiasi cha Bahari ya Baltiki katika upande wa kaskazini mwa Milima ya Carpathi kusini mwa nchi. Ndani ya eneo hilo lililo tupu, ardhi inatofautiana kutoka mashariki na magharibi.
Pwani ya Kipolandi ya Bahari ya Baltiki ni murua zaidi, lakini ina bandari asilia katika mkoa wa Gdańsk-Gdynia na Szczecin huko mashariki-magharibi ya mbali. Pwani hiyo ina upepo mzuri na maeneo kadhaa ya pwani za maziwa. Pwani za maziwa na fukwe za zamani ambazo zimekatwa kutoka baharini. Sehemu hizi pia huitwa rasi. Rasi ya Szczecin ipo upande wa mashariki mwa mpaka wa nchi ya Ujerumani. Rasi ya Vistula ipo upande wa mashariki mwa mpaka wa mji wa Kaliningrad, ambao ni katika mkoa wa Urusi.
Mto mrefu zaidi nchini Poland ni Vistula, unaoangukia ndani ya Rasi ya Vistula na pia unakwenda moja kwa moja hadi katika Bahari ya Baltiki. Ni km 1064 kutoka chanzo hadi mdomo.
Kanda ya kaskazini-mashariki ni miti tu imejaa, inakosa watu wachache na rasilimali za kilimo na viwanda. Kanda ya kijografia ina wilaya nne za vilima vya moraine na maziwa yaliyotengenezwa na moraine. Haya yalianzishwa baada ya Pleistocene Zama za Barafu. Ziwa Masurian ni miongoni mwa maziwa manne ya wilaya yaliyochukua eneo kubwa la kaskazini-mashariki mwa Poland.
Poland ina maziwa kibao. Kwa Ulaya nzima, Finland peke yake ina maziwa mengi zaidi. Maziwa makubwa ni "Śniardwy" na "Mamry". Kwa kuongeza katika wilaya ya ziwa katika kaskazini, kuna idadi kubwa pia ya mlima maziwa katika milima ya Tatra.
Kusini mwa kanda ya kaskazini-mashariki mwa mikoa ya Silesia na Masovia, ambapo kuna alama za mto na mabonde ya zama za barafu. Mkoa wa Silesia una rasilimali nyingi na watu wengi. Kuna makaa ya mawe tele. Silesia ya Chini ina mgodi wa shaba mkubwa kabisa. Tambarare ya Masovian ipo kati ya Poland. Ipo katika mabonde ya mito mikubwa mitatu: Vistula, Bug na Narew.
Ukiendelea na safari kusini ni mlima ya kanda ya Kipolandi. Milima hiyo ni pamoja na Sudetes na Milima ya Carpathi. Sehemu ndefu ya Carpathia ni milima ya Tatra ambayo imekwenda hadi kusini mwa mpaka wa nchi ya Poland.
Mlima mrefu zaidi nchini Poland unaitwa "Rysy" wenye m 2,503 (ft 8,210), upo Tatras.
Historia
Waslavi walienea kati nchi katika nusu ya pili ya karne ya 5 BK.
Ukristo wa Kikatoliki kupokewa na mfalme Mieszko I (960-992) na Wapolandi kwa jumla (966) hutazamiwa kama chanzo cha taifa lao la pekee katika jamii ya Waslavi.
Nchi ilistawi na kuenea hasa chini ya ukoo wa Jageloni (1386–1572).
Kuanzia mwaka 1764 nchi ilianza kurudi nyuma na zile za jirani ziligawana kwa awamu tatu (1772, 1793, 1795) eneo lake lote.
Wapolandi walijaribu mara kadha kujikomboa, lakini walipata uhuru kwa muda tu (1807-1815 na 1918-1939).
Baada ya vita vikuu vya pili, Polandi ikawa chini ya utawala wa Kikomunisti hadi ilipofaulu kujikomboa (1989).
Poland imekuwa nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu tarehe 1 Mei 2004.
Watu
Wakazi ni 38,483,957, karibu wote wakiwa Wapolandi asili (93.52%), wakiongea Kipolandi na wakifuata Ukristo katika Kanisa Katoliki (87.5%), tena kwa bidii ya pekee.
Kati ya lugha nyingine zilizotambulika kisheria, zinaongoza Kikashubi na Kijerumani, halafu Kibelarusi na, Kiukraina. Kati ya lugha za kigeni zinaongoza Kiingereza na Kirusi.
Tazama pia
Marejeo
Viungo vya nje
Kurasa za taasisi za serikali
- (Kipoland) (Kiingereza) Sejm - Sejm - lower chamber of the Parliament
- (Kipoland) (Kiingereza) Senat - Senate - upper chamber of the Parliament
- (Kipoland) (Kiingereza) Prezydent - President of the Republic of Poland
- (Kipoland) (Kiingereza) KPRM - Prime Minister's Office
- (Kipoland) (Kiingereza) Sąd Najwyższy - Supreme Court
- (Kipoland) (Kiingereza) (Kifaransa) Trybunał Konstytucyjny - Constitutional Tribunal
- (Kipoland) (Kiingereza) National Bank of Poland
- (Kipoland) (Kiingereza) The Poland.pl portal
- (Kipoland) (Kiingereza) Soko la Hisa la Warshawa
- (Kipoland) (Kiingereza) GUS - Central Statistical Office
- (Kipoland) (Kiingereza) Constitution of Poland
Utalii Poland
- Polish Guide of the Ministry of Foreign Affairs (poland.gov.pl)
- Polish National Tourist Office (poland-tourism.pl, a part of pot.gov.pl)
- Poland travel guide kutoka Wikisafiri
- Parks in Poland National parks, wetlands, biosphere reserves and other protected areas
Kurasa mtandaoni juu ya Poland
- Dobranoc - Free English to Polish Translation Services
- poland.gov.pl - the governmental page about Poland for international visitors
- Centreurope.org: Poland section
- World History Database Chronology of Poland
Habari za Poland kwa Kiingereza
- Warsaw Voice, an English-language newspaper
- Warsaw Business Journal, an English-language newspaper
- PolBlog - Polish News Site
- - Google News listing stories about Poland
Nchi za Umoja wa Ulaya | |
---|---|
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi |
Makala hii kuhusu maeneo ya Poland bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Polandi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |