Slovakia : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
No edit summary
Mstari 85: Mstari 85:
[[Jamii:Slovakia| ]]
[[Jamii:Slovakia| ]]
[[Jamii:Nchi za Umoja wa Ulaya]]
[[Jamii:Nchi za Umoja wa Ulaya]]
[[Jamii:Mkataba wa Schengen]]
[[Jamii:Nchi za Ulaya]]
[[Jamii:Nchi za Ulaya]]

Pitio la 17:09, 13 Desemba 2020

Slovakia

Slovakia (kwa Kislovakia: Slovensko) ni nchi ya Ulaya ya Kati yenye wakazi milioni tano na nusu.

Imepakana na Ucheki, Austria, Poland, Ukraine na Hungaria.

Slovakia imekuwa nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu tarehe 1 Mei 2004.

Mji mkubwa na mji mkuu ni Bratislava.

Miji muhimu baada ya Bratislava ni Košice, Banská Bystrica, Žilina, Trenčín, Nitra, Prešov na Trnava.

Wakazi walio wengi wanasema Kislovakia, ambacho ni kati ya lugha za Kislavoni, lakini kieneo kuna pia wasemaji wa Kihungaria, Kibelarus na Kiukraine.

Upande wa dini, 65.8% ni Wakatoliki, 8.9% Waprotestanti. 13.4% wanajitambulisha kama Wakanamungu.

Historia

Kwa sehemu kubwa ya historia yake hadi mwaka 1918 Slovakia ilikuwa chini ya watawala wa Habsburg waliokuwa wafalme na makaisari wa Austria.

Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia Slovakia ilipata uhuru pamoja na Ucheki katika nchi ya Chekoslovakia.

Mwaka 1993 Ucheki na Slovakia ziliachana kwa amani na kuwa kila moja nchi ya pekee.

Viungo vya nje


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Slovakia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.