Biashara : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d #WPWP,#WPWPTZ
d #WPWP,#WPWPTZ
Mstari 1: Mstari 1:
[[Picha:A man is selling biscuit.jpg|thumb|250|Mwanaume akiuza biskuti]]
[[Picha:A man is selling biscuit.jpg|thumb|350|Mwanaume akiuza biskuti]]
'''Biashara''' (kutoka [[neno]] la [[Kiarabu]]) ni shughuli au mchakato wa kununua na kuuza [[mali]] au [[Kitu|vitu]]. Inaweza kufanywa na mtu binafsi au kwa ushirikiano au na [[jamii]] au nchi kwa jumla.
'''Biashara''' (kutoka [[neno]] la [[Kiarabu]]) ni shughuli au mchakato wa kununua na kuuza [[mali]] au [[Kitu|vitu]]. Inaweza kufanywa na mtu binafsi au kwa ushirikiano au na [[jamii]] au nchi kwa jumla.



Pitio la 14:17, 20 Julai 2020

Mwanaume akiuza biskuti

Biashara (kutoka neno la Kiarabu) ni shughuli au mchakato wa kununua na kuuza mali au vitu. Inaweza kufanywa na mtu binafsi au kwa ushirikiano au na jamii au nchi kwa jumla.

Umiliki

Ingawa umiliki wa aina ya biashara hutofautiana kwa mujibu wa sheria, kuna aina kadhaa za kawaida:

  • Biashara ya mtu binafsi: ni biashara inayomilikiwa na mtu mmoja. Mmiliki anaweza kuiendesha biashara hii yeye binafsi au pia anaweza kuwaajiri wafanyikazi kumsaidia. Mmiliki wa biashara ina dhima ya binafsi ya madeni inayodaiwa biashara.
  • Biashara ya ushirikiano: ni aina ya biashara inayomilikiwa na watu wawili au zaidi kwa pamoja. Katika aina nyingi za ushirikiano , kila mmiliki ana dhima ya binafsi ya madeni yanayodaiwa biashara yao.
  • Kampuni: ni aina ya biashara ambapo wamiliki wa biashara zenyewe hawana dhima ya kibinafsi ya madeni ya biashara yenyewe. Biashara inaweza kuwa ya kutafuta faida au isiwe ya kutafuta faida. Kampuni nyingi zinamilikiwa na wenye hisa na shughuli zake husimamiwa na bodi ya wakurugenzi, ambayo huwaajiri wasimamizi wa biashara yenyewe. Pia kuna kampuni zinazomilikiwa na serikali mbali na zile zinazomiliokiwa na watu binafsi.
  • Vyama vya Ushirika: ni aina ya biashara ambayo pia kama kampuni wamiliki wake hawana dhima ya kibinafsi kwa madeni ya biashara ambayo lengo lake ni kutafuta faida au isiwe ya kutafuta faida. Vyama vya Ushirika hutofautiana na kampuni kwa kuwa vina wanachama, kinyume na wenye hisa katika kampuni, ambao hushirikishwa katika maamuzi ya chama chenyewe. Vyama vya ushirika kwa kawaida hugawanywa kamaVyama vya Ushirika vya wateja au Vyama vya Ushirika vya Wafanyikazi . Vyama vya ushirika ni mojawapo ya misingi wa itikadi ya demokrasia ya kiuchumi.

Aina za Biashara

Kuna aina nyingi za biashara, na kwa sababu hiyo, biashara huwekwa kwenye makundi kwa kutumia njia nyingi. Moja ya aina hizi inalenga shughuli za msingi za kibiashara zinazozalisha faida kwa biashara yenyewe:

  • Kilimo na biashara ya uchimbaji madini hushughulika na uzalishaji wa malighafi, kama vile mimea au madini.
  • Soko la fedha ni pamoja na mabenki na makampuni mengine ambayo huzalisha faida kupitia uwekezaji na usimamizi wa fedha za uwekezaji.
  • Biashara za habari huzalisha faida kutokana mauzo ya hakimiliki na ni pamoja na biashara za video, wachapishaji na makampuni ya kuunda programu za tarakilishi.
  • Watengenezaji bidhaa viwandani huzalisha bidhaa kutoka malighafi au sehemu ya bidhaa, kisha huuza kwa faida. Makampuni ambayo huunda bidhaa, kama vile magari au mabomba, huchukuliwa kama watengenezaji wa bidhaa.
  • Biashara isiyohamishika huzalisha faida kutokana na kuuza, kukodisha, na maendeleo ya mali, nyumba, na majengo.
  • Wauzaji wa bidhaa za rejereja na wasafirishaji wa bidhaa zenyewe huingilia kati shughuli ya kuzitoa bidhaa kutoka kwa watengenezaji hadi kwa wateja na kuzalisha faida kutokana na mauzo au usambazaji na kutoa huduma. Wengi wa wafanyabiashara wanaoshughulikia wateja moja kwa moja ni wasafirishaji wa bidhaa au wauzaji wa rejareja (kwa Kiingereza: Retailing). Wako wafanyabiashara wa rejareja wanaolenga soko maalum kama vile wale wanaouza biashara za anasa kwa mamilionea[1].
  • Biashara za kutoa Huduma ni biashara ambazo hupata faida yake kutokana na kutoa huduma fulani kwa wateja wake. Mashirika kama vile makampuni ya ushauri, mikahawa na hata watumbuizaji ni aina ya biashara za huduma. Pia kuna mshipuko mpya wa biashara za kutafutia wat kazi na vibarua ambazo pia ni biashara za kutoa huduma.[2]
  • Biashara ya Usafiri ni biashara ambayo hupata faida yake kupitia kuwasafirisha watu na bidhaa kutoka mahali pamoja hadi mahala pengine.
  • Pia kuna makampuni yanayotoa huduma ya umma, kama vile joto, umeme, au uzoaji taka, na kwa kawaida huwa ni mashirika ya kiserikali.

Kuna migawanyiko mingine mingi ya aina za biashara[3].

Usimamizi

Ufanisi wa uendeshaji wa biashara, na kujifunza somo hili, huitwa usimamizi. Matawi makuu ya usimamizi ni: usimamizi wa fedha, usimamizi wa masoko, usimamizi wa rasilimali watu, usimamizi wa mikakati, usimamizi wa uzalishaji, usimamizi wa huduma na usimamizi wa teknolojia ya habari.

Kurekebisha Mashirika ya Kitaifa

Katika miongo ya hivi karibuni, mali na makampuni ambayo yalikuwa yakiendeshwa na mataifa mbalimbali yamekuwa yamebadilishwa na kufuata mtindo wa makampuni ya kibiashara. Katika mwaka wa 2003, Jamhuri ya Watu wa Uchina ilibadilisha 80% ya makampuni yanayomilikiwa na serikali na kuyaweka kwenye mfumo sawa na mashirika ya kibiashara.[4]

Usimamizi wa Serikali

Benki Kuu ya England katika Threadneedle Street, London, Uingereza.

Mamlaka nyingi hutoa sheria zinazoelekeza umiliki wa biashara na jinsi biashara inavyoendeshwa katika taifa husika.

Mpangilio

Mambo makubwa yanayoathiri mpangilio wa biashara ni kama vile:

  • Ukubwa wa biashara na matarajio ya usimamizi na umiliki. kwa ujumla biashara ndogo zinaweza kubadilika kwa urahisi , ilhali biashara kubwa, au zile zenye umiliki mpana au miundo rasmi, kwa kawaida upangiliwa kama ubia au makampuni. Aidha biashara ambayo inataka kuongeza fedha kwenye soko la hisa au kuwa inamilikiwa na watu anuwai mara nyingi inatakiwa upangile kwa mfumo maalumu wa kisheria ili kufanya hivyo.
  • Sekta na nchi. Biashara za binafsi zenye malengo ya kupata faida ni tofauti na biashara zinazomilikiwa na serikali. Katika baadhi ya nchi, baadhi ya biashara ni wajibu wa kisheria na mpangilio fulani.
  • Dhima ya binafsi. Makampuni na baadhi ya biashara zingine huwalinda wamiliki wake dhidi ya kupoteza mali yao wakati biashara inaposhindwa kulipa madeni yake kwa kuifanya kiungo tofauti na wao wenyewe kinacho tambulika kisheria. Kwa kulinganisha, biashara zingine zilizomilikiwa na watu binafsi au na idadi chache ya watu huwa hazijalindwa hivi kisheria.
  • Faida katika ulipaji wa kodi. Miundo tofauti tofauti katika sheria za kodi hushughulikiwa vitofauti, na huenda jambo hili likailetea biashara yenyewe faida.
  • Mahitaji ya uwazi. Miundo tofauti ya biashara huitajika kutoa kiwango fulani cha habari kwa umma (au kuripoti kwa mamlaka husika),na huitajika kutimiza marshati tofauti tofauti.

Watu wawili au zaidi wanaoendesha biashara kwa pamoja lakini wameshindwa kuandaa jinsi maalum ya kujiendesha, wataonekana kama ushirikiano wa ujumla. Sheria ya ushirika ni sehemu ya usimamizi kwa makubaliano ya ushirikiano ikiwa moja imeundwa, na sehemu kwa sheria ya mamlaka ambapo ushirikiano hupo.

Mtu binafsi nayemiliki na kuendesha biashara anajulikana kama mmiliki pekee awe ameimiliki kupitia kwa njia rasmi au vingine.

Vipengele vichche muhimu vya kuzingatia katika kuamua jinsi ya kuendesha biashara ni pamoja na:

  1. Baadhi ya wamiliki wa biashara katuika mpango wa pamoja huwa wana dhima ya kibanafsi na wanalipia gharama yoyote inayosababishwa na kutolipa kwa madeni yanayodaiwa biashara.
  2. Kwa ujumla, makampuni huhitajika kulipa kodi kama watu "halisi" . Katika baadhi ya mifumo ya kodi, hii inaweza kuleta hali inayojulikana kama kodi maradudfu kwa sababu kwanza biashara hulipia kodi ya faida, na kisha wakati shirika linasambaza faida zake kwa wamiliki wake, watu binafsi pia hulipa kodi ya mapato.
  3. Katika nchi nyingi, kuna sheria ambazo huchukulia makampuni makubwa makubwa tofauti na biashara dogo dogo. Zinaweza kuepuka kutimiza marshati fulani,kurahisishwa kwa baadhi ya shughuli na njia tofauti ya kulipa kodi.
  4. "Kwenda umma" (wakati mwingine huitwa IPO) - ambayo ina maana ya kuruhusu sehemu ya biashara kuwa inamilikiwa na wawekezaji kwa upana au wananchi kwa ujumla-ni lazima kuandaa mfumo tofauti, ambayo ni kawaida ya sheria na taratibu.

Sheria za biashara

Shughuli nyingi za kibiashara hufuata sheria maaalum ambazo zimechukua muda mrefu kuuundwa na zinaendelea kurekebishwa kulingana na hali halisi.

Kama sheria nyingine zinazoadhiri shughuli za kibiashara, katika nchi nyingi ni vigumu kuzirejelea sheria hizi katika mahala pamoja. Kuna sheria zinazosimamia mambo ya kazi na kwa ujumla mahusiano na wafanyakazi, usalama na masuala ya ulinzi ('OSHA' au Afya na Usalama), sheria za kutobagua (umri, jinsia, ulemavu, kabila, na katika baadhi ya utawala, maswala ya ngono), mshahara wa chini kabisa, muungano wa sheria, sheria za fidia ya wafanyakazi, na likizo za kimwaka au wakati wa kazi.

Katika baadhi ya biashara maalumu, kuna leseni maalum zinazoitajika, aidha kutokana na sheria maalum kujihusisha na biashara fulani, kazi au taaluma, ambayo inaweza kuhitaji elimu maalumu, au kwa serikali za mitaa. Taaluma ambazo zinahitaji leseni maalumu mbalimbali ni kama vile sheria, udaktari, kuuza vileo, rubani, utangazaji redio, kuuza dhamana za uwekezaji, kuuza magari yaliyotumika na kadhalika. Sheria za serikali za mitaa pia zinahitaji leseni na kodi maalum ili kuendesha biashara ya aina yoyote.

Baadhi ya biashara ziko chini ya sheria zinazoendelea kuundwa. Hizi ni pamoja na viwanda, kwa mfano, huduma za umma, uwekezaji amana, benki, bima, utangazaji, anga, na watoa huduma za afya. Kanuni za mazingira pia ni ngumu sana na zinaweza kuathiri biashara za aina nyingi katika njia zisizotarajiwa.

Fedha za kuanzisha na kuendesha biashara

Wakati biashara zinataka kuchangisha fedha fedha (iitwayo 'mtaji'), sheria zaidi huhusika. Sheria na kanuni nyingi huelekeza jinsi ya kuuza dhamana za uwekezaji (njia ya kuongeza fedha) katika nchi nyingi za Magharibi. Kanuni hizi zinaweza kuhitaji kuweka wazi mambo mengi kuhusiana na maswala ya kifedha ya kampuni husika na hivyo kuwapa wanunuzi 'remedies'. Kwa sababu "dhamana" ni neno pana sana, shughuli nyingi za uwekezaji huweza kuwa chini ya sheria hizi, isipokuwa katika visa maalum.

Fedha zinaweza kupatikana kupitia njia za binafsi, kwa kutoa hisa kwa umma ('IPO') kwenye soko la hisa, au kwa njia nyingine nyingi. Baadhi ya masoko ya hisa ni kama vile Shanghai Stock Exchange, Singapore Exchange, Hong Kong Stock Exchange, New York Stock Exchange na Nasdaq (Marekani), London Stock Exchange (Uingereza), wa Tokyo Stock Exchange (Ujapani), na kadhalika.

Biashara ambazo zimefanywa za "umma" na usimamamizi mwingi sana kuhusu utawala wa ndani (kama jinsi malipo ya maafisa watendaji hudhamiriwa) na wakati na jinsi habari ni wazi kwa umma zao na wanahisa. Huko Marekani, kanuni hizi za kimsingi kusisitizwa na kutekelezwa na 'United States Securities and Exchange Commission' (SEC). Mataifa mengine ya Magharibi yana viungo vya udhibiti vwa kulinganishwa na hiki. Kanuni hizi husisitizwa na kutekelezwa na 'China Securities Regulation Commission' (CSRC), huko Uchina. Huko Singapore, mamlaka ya udhibiti ni 'Monetary Authority of Singapore' (MAS), na huko Hong Kong, ni 'Securities and Futures Commission' (SFC).

Ni vigumu sana kuzitaja sheria zote ambazo huathiri biashara. Kwa kweli, sheria hizi zimekuwa nyingi hadi kwamba hakuna mwanasheria yeyote wa biashara anayeweza kujifunza zote, na kulazimisha kampuni kuongeza umaalumu miongoni mwa wanasheria wake. Ni jambo la kawaida kwa wanasheria 5-10 kuhitajika hili kushughulikia aina fulani ya shughuli ya kibiashara, kutokana na jinsi sheria za kuelekeza biashara zilivyo nyingi. Sheria za kibiashara huhusu sheria za ushirika za ujumla, sheria ya ajira na kazi, afya, dhamana, 'M & A' (ambaye anashughulikia mambo ya ununuzi), kodi, 'ERISA'(ERISA Marekani inahusiana na mipango ya faida ya mfanyakazi), chakula na madawa ya udhibiti, umiliki (hushughulika na 'copyrights', ruhusa, 'Trademarks' na kadhalika), sheria ya mawasiliano ya simu, na zaidi.

Nchini Thailand, kwa mfano, ni lazima kujiandikisha kiasi fulani cha mtaji kwa kila mfanyakazi, na kulipa ada kwa serikali kwa kiwango cha mtaji kilichoandikishwa. Hakuna mahitaji ya kisheria kuthibitisha kuwa mtaji huu kweli hupo, kinachoitajika pekee ni kulipa ada yenyewe.

Umiliki

Wafanyabiashara mara nyingi huwa na umiliki muhimu ambao unahitaji ulinzi dhidi ya washindani ili kuzidi kupata faida. Hii inaweza kuhitaji 'patent' au 'copyrights' au utunzaji wa siri za biashara ('trade secrets'). Wafanyabiashara wengi wana logo na mbinu ambazo zinaweza kuwafaidi katika 'trademarking'. Kwa sababu ya asili ya haki miliki, wanahitaji ulinzi wa biashara katika kila mamlaka ambamo wana wasiwasi kuhusu washindani. Nchi nyingi zimetia saini mikataba ya kimataifa kuhusu haki miliki, hivyo makampuni yaliyosajiliwa katika nchi hizo chini ya sheria za kitaifa zimefungwa na mikataba hiyo pia.

Mipango ya Kutoka

Biashara zinaweza kununuliwa na kuuzwa. Mara nyingi wamiliki biashara urejelea mpango wao wa kutoka kwenye biashara kama "mpango wa kutoka" ('exit plan'). Mipango hii mingi ni pamoja na IPO, MBO na kuungana na biashara nyingine. Biashara mara nyingi hazifutiliwi mbali, kwani kufanya hivyo mara nyingi huwa na hasara kubwa.

Marejeo

  1. Bidhaa za anasa
  2. Vested Technology (8 March 2018). Temp to Hire (en-US). Vested Technology Website. Iliwekwa mnamo 19 July 2018.
  3. Types of business structures,State of Washington,Business Licence Service;bls.dor.wa.gov/ownershipstructures.aspx
  4. http://english.people.com.cn/data/China_in_brief/Economy/Major% 20Industries.html

Viungo vya nje

Jua habari zaidi kuhusu Business kwa kutafuta kupitia mradi wa Wikipedia Sister
Uchambuzi wa kamusi kutoka Wikamusi
Vitabu kutoka Wikitabu
Dondoo kutoka Wikidondoa
Matini za vyanzo kutoka Wikichanzo
Picha na media kutoka Commons
Habari kutoka Wikihabari
Vyanzo vya elimu kutoka Wikichuo
Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Biashara kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.