Baharia : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sahihisho kamili na kuondoa maneno ya kihuni!
d Protected "Baharia": Kuna wimbi la upotovu wa lugha rasmi ya Baharia nchini Tanzania. Kuondoa shaka ya kuvurugwa kimaana, nimefunga ukurasa huu kwa muda wa mwaka. ([Kuhariri=Ruhusa kwa wakabidhi tu] (itakwisha 07:39, 10 Septemba 2020 (UTC)) [Kuhamisha=Ruhusa kwa wakabidhi tu] (itakwisha 07:39, 10 Septemba 2020 (UTC)))
(Hakuna tofauti)

Pitio la 07:39, 10 Septemba 2019

Mabaharia wakiangalia kung'oa kwa nanga wakati wa kutoka bandarini
Mabaharia Wajerumani kwenye kazi ya usafi wa sitaha kwenye jahazi mnamo 1958

Baharia, pia mwanamaji ni mtu anayefanya kazi kwenye chombo cha usafiri majini, hasa baharini kama vile boti, mashua, jahazi au meli. "Mwanamaji" hutumiwa mara nyingi kwa kutaja mabaharia wa kijeshi.

Kuna kazi nyingi tofauti zinazotekelezwa na mabaharia. Mkuu wao ni nahodha au kapteni wa chombo. Katika mashua au jahazi ndogo mabaharia wote wanafanya kazi pamoja ilhali kazi sahili na ngumu zaidi hupewa kwa wale walio vijana. Kadri jinsi meli ni kubwa zaidi shughuli zinagawiwa baina ya mabaharia wenye ufundi fulani.

Meli kubwa unaweza kuwa na idara tofauti kama vile

  • shughuli za sitaha pamoja na mizigo
  • shughuli za injini
  • huduma za chakula
  • huduma ya afya

Hapo kapteni atakuwa na kundi la maafisa wake wanaosimamia idara mbalimbali baada ya kupita kwenye mafunzo na mitihani maalumu kwa ajili ya shughuli zao.

Viungo vya Nje