Kitabu cha Mhubiri : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
→‎Viungo vya nje: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Mstari 21: Mstari 21:


==Viungo vya nje==
==Viungo vya nje==
*[https://www.jw.org/sw/machapisho/biblia/nwt/vitabu/mhubiri/ Mhubiri (Tafsiri ya Ulimwengu Mpya)]
*[https://www.jw.org/sw/machapisho/video/utangulizi-wa-biblia/kitabu-cha-mhubiri/ Utangulizi wa Mhubiri]
*[http://www.biblephone.net/mobile/index.php/swa/2/Eccles/ Kitabu cha Mhubiri katika [[tafsiri]] ya [[Kiswahili]] (Union Version)]
*[http://www.biblephone.net/mobile/index.php/swa/2/Eccles/ Kitabu cha Mhubiri katika [[tafsiri]] ya [[Kiswahili]] (Union Version)]



Pitio la 13:56, 5 Septemba 2018

Mhubiri (pia: Koheleti) ni kimojawapo kati ya vitabu vya hekima vilivyomo katika Tanakh (Biblia ya Kiebrania) na hivyo pia katika Agano la Kale la Biblia ya Kikristo. Kwa sababu hiyo kilidhaniwa kimeandikwa na mfalme Solomoni, kielelezo cha hekima katika Biblia.

Kitabu hicho kina sura kumi na mbili na kwa kiasi kikubwa kimeandikwa kwa njia ya ushairi.

Jina

Katika lugha ya Kiebrania jina lake ni קֹהֶלֶת (Qohelet), maana yake "Mhadhiri": ndivyo anavyojiita mwandishi, ambaye hajulikani kwa jina.

Mada

Yeye anakabili masuala ya maisha kwa kuzingatia upande chanya na upande hasi wa kila moja ili kufikia hekima.

Hasa anajiuliza juu ya maana ya maadili wakati ufunuo wa Mungu ulikuwa haujafikia hatua ya kufundisha uzima wa milele na maisha yalikuwa yanaonyesha mara nyingi ustawi wa waovu na hali ngumu ya waadilifu.

Mbele ya utovu wa haki duniani, Mhubiri alikariri, "Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili" (1:2).

Hata hivyo, hatimaye akajumlisha mawazo yake kwa kuhimiza kwa imani, "Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu. Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya" (12:13-14).

Ufafanuzi

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Maendeleo hayo yataweka wazi kwamba hukumu itafanyika baada ya kifo, na kwamba tuzo na [[]]adhabu vitatolewa kwa haki katika uzima wa milele.

Viungo vya nje

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.