Ruaha Mkuu : Tofauti kati ya masahihisho
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 12: | Mstari 12: | ||
[[File:Dry Great Ruaha River and.jpg|thumb||Ruaha Mkuu jinsi ilivyokauka mwaka [[2006]] kwenye eneo la [[Hifadhi ya Ruaha|Hifadhi ya taifa ya Ruaha]].]] |
[[File:Dry Great Ruaha River and.jpg|thumb||Ruaha Mkuu jinsi ilivyokauka mwaka [[2006]] kwenye eneo la [[Hifadhi ya Ruaha|Hifadhi ya taifa ya Ruaha]].]] |
||
Maji ya Ruaha Mkuu ni muhimu kwa [[ekolojia]] ya [[beseni]] lake pamoja na [[watu]] wote wanaoishi huko. Lakini matumizi ya [[binadamu]] yameleta mvurugo kwa ekolojia ya mto na tangu mwaka [[1993]] mto umeanza kukauka wakati wa [[ukame]]. Uhaba wa maji umesababishwa na matumizi mabaya ya maji upande wa miradi mikubwa ya [[mpunga]] katika Usangu. |
Maji ya Ruaha Mkuu ni muhimu kwa [[ekolojia]] ya [[beseni]] lake pamoja na [[watu]] wote wanaoishi huko. Lakini matumizi ya [[binadamu]] yameleta mvurugo kwa ekolojia ya mto na tangu mwaka [[1993]] mto umeanza kukauka wakati wa [[ukame]]. Uhaba wa maji umesababishwa na matumizi mabaya ya maji upande wa miradi mikubwa ya [[mpunga]] katika Usangu. |
||
==Tazama pia== |
|||
* [[Mito ya Tanzania]] |
|||
* [[Orodha ya mito ya mkoa wa Morogoro]] |
|||
==Tanbihi== |
==Tanbihi== |
||
Mstari 17: | Mstari 21: | ||
==Viungo vya nje== |
==Viungo vya nje== |
||
* [http://www.geonames.org Geonames.org] |
|||
* [http://www.wwf.org.uk/filelibrary/pdf/ruaha.pdf WWF.org - The Ruaha Water Programme] |
* [http://www.wwf.org.uk/filelibrary/pdf/ruaha.pdf WWF.org - The Ruaha Water Programme] |
||
* [http://www.adventurecamps.co.tz/ruahainfo.htm Ruaha information with images] |
* [http://www.adventurecamps.co.tz/ruahainfo.htm Ruaha information with images] |
Pitio la 15:42, 1 Mei 2018
Ruaha Mkuu (pia: Ruaha Mkubwa) ni mto muhimu nchini Tanzania na tawimto wa Rufiji. Huitwa "Ruaha Mkuu" kwa kuutofautisha na "Ruaha Mdogo" unaoishia ndani yake, si mbali na Iringa Mjini. Jina Ruaha kwa Kihehe linamaanisha "maji mengi".
Chanzo na mwendo wa mto
Chanzo chake ni mito mingi midogo inayotelemka milima ya nyanda za juu za kusini mwa Tanzania, hasa safu za milima ya Uporoto na ya Kipengere. Mito hii inakusanya maji yake kwenye tambarare ya Usangu na ndipo Ruaha inapoanza. Mito mikubwa zaidi inayoungana hapa na kuunda Ruaha ni pamoja na mto Mbarali, mto Kimani na mto Chimala.
Karibu na Ng’iriama mto unatoka katika Usangu na kuingia hifadhi ya kitaifa ya Ruaha. Inaendelea kupokea Ruaha Mdogo na mto Kisigo kabla ya kuingia katika ziwa la lambo la Mtera, halafu inaendelea hadi lambo la Kidatu.
Baada ya Kidatu, Ruaha Mkuu unapita tambarare ya Kilombero hadi kuishia katika mto Rufiji.
Matatizo ya ekolojia ya mto
Maji ya Ruaha Mkuu ni muhimu kwa ekolojia ya beseni lake pamoja na watu wote wanaoishi huko. Lakini matumizi ya binadamu yameleta mvurugo kwa ekolojia ya mto na tangu mwaka 1993 mto umeanza kukauka wakati wa ukame. Uhaba wa maji umesababishwa na matumizi mabaya ya maji upande wa miradi mikubwa ya mpunga katika Usangu.
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
- Geonames.org
- WWF.org - The Ruaha Water Programme
- Ruaha information with images
- FAO review
- FAO - fact sheet on the ecohydrology of the Great Ruaha River (2003)
Öhman, May-Britt, Taming Exotic Beauties: Swedish Hydro Power Constructions in Tanzania in the Era of Development Assistance, 1960s - 1990s, Stockholm, 2007, PhD Thesis, http://www.diva-portal.org/smash/record.jsf?pid=diva2:12267
Coordinates: 7°56′S 37°52′E / 7.933°S 37.867°E
Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Ruaha Mkuu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |