Nzi (kundinyota) : Tofauti kati ya masahihisho
No edit summary |
|||
Mstari 6: | Mstari 6: | ||
==Jina== |
==Jina== |
||
Nzi ni kati ya kundinyota zilizobuniwa tangu mabaharia Wazungu kuzunguka dunia yote yaani karne ya 16. Hazikujulikani kwa Wagiriki wa Kale au Waarabu waliojifunza kutoka kwao. Kundinyota hii ilielezwa mara ya kwanza na mabaharia Waholanzi [[Pieter Dirkszoon Keyser]] na Frederick de Houtman katika safari yao ya kuelekea [[Indonesia]] zikaonyeshwa mara ya kwanza mwaka 1598 katika |
Nzi ni kati ya kundinyota zilizobuniwa tangu mabaharia Wazungu kuzunguka dunia yote yaani karne ya 16. Hazikujulikani kwa Wagiriki wa Kale au Waarabu waliojifunza kutoka kwao. Kundinyota hii ilielezwa mara ya kwanza na mabaharia Waholanzi [[Pieter Dirkszoon Keyser]] na Frederick de Houtman katika safari yao ya kuelekea [[Indonesia]] zikaonyeshwa mara ya kwanza mwaka 1598 katika [[globu ya nyota]] ya [[Petrus Plancius]]. |
||
Keyser alitumia jina la [[Kiholanzi]] De Vlieghe ([[Nzi]]) iliyotajwa baadaye kwa jina la Kilatini „Musca“. Baadaye ilipokelewa katika "Uranometria" ya [[Johann Bayer]] aliyetumia njia ya "Apis" (nyuki) na hivyo kuna vitabu vya zamani zinazotumia jina Apis lakini baadaye "Musca" ilirudishwa. |
Keyser alitumia jina la [[Kiholanzi]] De Vlieghe ([[Nzi]]) iliyotajwa baadaye kwa jina la Kilatini „Musca“. Baadaye ilipokelewa katika "Uranometria" ya [[Johann Bayer]] aliyetumia njia ya "Apis" (nyuki) na hivyo kuna vitabu vya zamani zinazotumia jina Apis lakini baadaye "Musca" ilirudishwa. |
Pitio la 19:01, 8 Oktoba 2017
Nzi (kwa Kilatini na Kiingereza Musca) [1] ni jina la kundinyota kwenye nusutufe ya kusini ya dunia yetu.
Mahali pake
Nzi iko jirani na kundinyota mashuhuri ya Salibu (Crux) iliyopo upande wa kaskazini, Mkuku (en:Carina) upande wa magharibi, Kinyonga (Chamaeleon) upande wa kusini , Ndege wa Peponi (Apus) na Bikari (Circinus) upande wa kaskazini-mashariki.
Jina
Nzi ni kati ya kundinyota zilizobuniwa tangu mabaharia Wazungu kuzunguka dunia yote yaani karne ya 16. Hazikujulikani kwa Wagiriki wa Kale au Waarabu waliojifunza kutoka kwao. Kundinyota hii ilielezwa mara ya kwanza na mabaharia Waholanzi Pieter Dirkszoon Keyser na Frederick de Houtman katika safari yao ya kuelekea Indonesia zikaonyeshwa mara ya kwanza mwaka 1598 katika globu ya nyota ya Petrus Plancius.
Keyser alitumia jina la Kiholanzi De Vlieghe (Nzi) iliyotajwa baadaye kwa jina la Kilatini „Musca“. Baadaye ilipokelewa katika "Uranometria" ya Johann Bayer aliyetumia njia ya "Apis" (nyuki) na hivyo kuna vitabu vya zamani zinazotumia jina Apis lakini baadaye "Musca" ilirudishwa.
Leo Musca iko pia kati ya kundinyota 88 zinazoorodheshwa na Umoja wa kimataifa wa astronomia [2] Kifupi chake rasmi kufuatana na Ukia ni 'Mus'.[3]
Nyota
Nyota angavu zaidi ni α Alfa Muscae yenye uangavu unaoonekana wa 2.7 mag ikiwa na umbali wa Dunia wa miaka ya nuru 310[4] Ni rahisi kuona maana ni ni yota angavu jirani na Salibu kwa kufuata mstari wa urefu wa salibu kuelekea kusini.
Tanbihi
- ↑ Uhusika milikishi (en:genitive) ya neno "Musca" katika lugha ya Kilatini ni "Muscae" na hili ni umbo la jina linaloonekana katika majina ya nyota za kundi hili kama vile Alfa Muscae, nk.
- ↑ The Constellations, tovuti ya International Astronomical Union , iliangaliwa Julai 2017
- ↑ Russell, Henry Norris (1922). "The New International Symbols for the Constellations". Popular Astronomy 30: 469–71. Bibcode:1922PA.....30..469R.
- ↑ Alphamus (Alpha Muscae), tovuti ya Prof. Jim Kaler, university of Illinois, iliangaliwa Oktoba 2017
Viungo vya Nje
- Constellation Guide: Musca constellation
- The Deep Photographic Guide to the Constellations: Musca
- Star Tales – Musca
- Richard Hinckley Allen: Star-Names and their Meanings; kwa G. E. Stechert New York, Leipzig, London, Paris 1899, ukurasa 336 ff (online kwenye archive.org)