Migoli : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d wa wa --> wa; new lines; double spaces using AWB
No edit summary
Mstari 1: Mstari 1:
'''Migoli''' ni [[mji mdogo]] kwenye [[Wilaya ya Iringa Vijijini]] katika [[Mkoa wa Iringa]], [[Tanzania]]. Iko mita 700 juu ya usawa wa bahari.
'''Migoli''' ni [[mji mdogo]] kwenye [[Wilaya ya Iringa Vijijini]] katika [[Mkoa wa Iringa]], [[Tanzania]] yenye [[Postikodi Tanzania|Postikodi namba]] 51221. Iko mita 700 juu ya usawa wa bahari.


Unapatikana kando ya [[Bwawa la Mtera]] ambako wakazi wengi hutegemeza maisha yao katika [[uvuvi]].
Unapatikana kando ya [[Bwawa la Mtera]] ambako wakazi wengi hutegemeza maisha yao katika [[uvuvi]].

Pitio la 06:53, 30 Septemba 2017

Migoli ni mji mdogo kwenye Wilaya ya Iringa Vijijini katika Mkoa wa Iringa, Tanzania yenye Postikodi namba 51221. Iko mita 700 juu ya usawa wa bahari.

Unapatikana kando ya Bwawa la Mtera ambako wakazi wengi hutegemeza maisha yao katika uvuvi.

Eneo hili lina rutuba lakini mvua ni chache (kwa kawaida haifikii mm. 300 kwa mwaka), hivyo wakazi hawajishughulishi sana na kilimo, hivyo wananunua nafaka kutoka sehemu ambazo zinalimwa kwa wingi, kama vile Ismani tarafani na Mtamba mkoa wa Dodoma.

Kumbe ni eneo maarufu kwa ufugaji, hasa wa ng'ombe na mbuzi, wanaostawi katika mbuga isiyo na malale.

Eneo hili, ambapo inapita barabara kuu ya Afrika kutoka Misri hadi Afrika Kusini (ingawa sehemu hii kati ya Dodoma na Iringa haimalizika kutiwa lami), ni endelevu hasa ukilinganishwa na vijiji vingine vya nchi ya Tanzania, kwa kuwa una huduma nyingi za jamii ambazo zimetokana na juhudi za serikali na wananchi wenyewe.

Wafadhili wa miradi mbalimbali ni kama vile parokia katoliki ya Migoli na makampuni ya mawasiliano kama vile Zain, Tigo, Vodacom na Zantel.

Kijiji asili kilikua sana baada ya serikali kuanza kujenga bwawa la Mtera na kulazimisha watu walioishi bondeni na pembezoni mwa mkondo wa mto Ruaha wasogee ikiwa ni miaka ya 1980. Wazee wa kwanza walioshi katika mitaa miwili ya Migoli na Makonge walikuwa Maulidi Ndilwa, Nyakunga, Simili Magomba, Paulo Magomba, Madekedeke, Kinyaga pamoja na familia zao.

Tangu kuanzishwa kwa Bwawa la Mtera na kijiji cha Migoli, shughuli ya uvuvi ilikikuza sana kijiji cha Migoli ambacho kimekuwa mahali pa biashara yaani watu kutoka makambini (makazi yasiyo rasmi ya uvuvi) walikuwa wakiuzia samaki kwenye kijiji cha Migoli.

Hata hivyo wafanyabiashara wa samaki wamekitumia kijiji cha Migoli kuwa sehemu yao ya kufikia kabla ya kwenda kwenye makambi. Makambi yanayokitegemea kijiji cha Migoli ni Nyegere, Mabati, Maperamengi, Mandela, Kilambakitali, Changalawe na mengine mengi.

Hatimaye kijiji kimemegwa na kuzaa kijiji kipya cha Mtera upande wa kaskazini.

Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ya Migoli ilikuwa na wakazi wapatao 10,937 waishio humo.[1]

Siku hizi barabara inayopita kijijini ikiunganisha Iringa na Dodoma, hivyo pia Cape Town na Kairo, imetiwa lami.

Marejeo

Kata za Wilaya ya Iringa Vijijini - Tanzania

Idodi | Ifunda | Ilolompya | Itunundu | Izazi | Kalenga | Kihanga | Kihorogota | Kising'a | Kiwere | Luhota | Lumuli | Lyamgungwe | Maboga | Magulilwa | Mahuninga | Malengamakali | Masaka | Mboliboli | Mgama | Migoli | Mlenge | Mlowa | Mseke | Nyang'oro | Nzihi | Ulanda | Wasa


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Iringa bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Migoli kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.