Lyiza
Lyiza ni filamu fupi ya mwaka 2011 ya Rwanda iliyoongozwa na Marie-Clementine Dusabejambo.
Muhtasari
[hariri | hariri chanzo]Yaliyopita bado yanaishi ndani ya maisha ya Lyiza ambaye analazimika kuishi na kumbukumbu ya kutisha ya mauaji ya wazazi wake, wakati wa mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi mwaka 1994 nchini Rwanda.[1] Anapomtambua baba wa mwanafunzi mwenzake, Rwena, mtu aliyehusika na mauaji yao, anasema hivyo hadharani, na kusababisha mvutano mkubwa. Lakini maelewano yanarudi kupitia uingiliaji kati wa mwalimu ambaye anawapeleka vijana kwenye jumba la makumbusho la mauaji ya kimbari, mahali pa kumbukumbu, na kumuongoza Lyiza kujifunza kusamahe. Bila kuwa na udadisi na kwa mtindo asilia wa masimulizi, filamu inasisitiza umuhimu wa kubadilishana uzoefu na kuelimisha kwa ajili ya ukweli na upatanisho.[3]