Lupus wa Sens

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Lupus wa Sens akigawa sadaka; mchoro mdogo wa karne ya 14.

Lupus wa Sens (au Loup wa Sens) (573 hivi - 623 hivi)[1] alikuwa askofu wa 19 wa Sens, Ufaransa.

Alikuwa mtoto wa Betton, kabaila wa Tonnerre, kutoka ukoo uliotawala Burgundy.[1] Kwa ushujaa wake alipelekwa uhamishoni[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Septemba[3][4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: