Leufridi
Leufridi (pia: Leutfridus, Leutfrido, Leufredo, Leutfrid, Leufroi, au Leufroy; alifariki Evreux, 738[1]) alikuwa mmonaki Mbenedikto wa Ufaransa, ndugu wa mtakatifu Agofredus na mwanafunzi wa mtakatifu Sidoni wa Saint-Saëns.
Maisha[hariri | hariri chanzo]
Leufridi alisoma katika abasia ya Condat na huko Chartres, akawa kwa muda fulani mwalimu huko Evreux.
Baada ya kuishi kama mkaapweke sehemu mbili tofauti, alianzisha monasteri ya La Croix-Saint-Qu'en mwaka 690 hivi, akawa abati wake wa kwanza na kuliongoza kwa miaka 48 hivi.[1]
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu[2].
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 21 Juni.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- St Leutfridus, Saint of Just and Holy Wrath, excerpt from a lecture given by Prof Plinio Corrêa de Oliveira on June 20, 1967
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |