Lango:Sanaa/Intro

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sanaa ni usanii wowote, yaani utendaji wa binafsi au wa pamoja ambao, kwa kutumia vipaji vya kuzaliwa navyo au mbinu zinazotokana na mang'amuzi na masomo, unabuni na kuleta uzuri. Sanaa imegawanyika sehemu nyingi: k.mf. muziki, uigizaji, uchezaji, uchoraji, upigaji picha, sinema, ushonaji, uhariri, uchongaji, uandishi, ushairi.