Nenda kwa yaliyomo

Landolphia owariensis

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Landolphia owariensis ni aina ya liana kutoka familia ya Apocynaceae inayopatikana katika maeneo ya tropiki barani Afrika. Maji-maziwa (latex) yanaweza kutolewa kutoka kwenye mmea huu kwa ajili ya kutengeneza mpira wa asili (kiing. natural rubber). Majina mengine ya mzabibu huu ni eta, mzabibu wa mpira mweupe, na mmea wa mpira wa Kongo[1]. Mpira wa Kongo ulikuwa bidhaa ya mpira wa biashara iliyokuwa ikisafirishwa kutoka Congo Free State kuanzia mwaka 1890, na unajulikana sana kwa jinsi ulivyokuwa ukivunwa kwa kulazimisha watu kufanya kazi katika mazingira ya mateso makubwa ya kibinadamu. Hali hii ilielezewa kwa kina katika Ripoti ya Casement ya mwaka 1904. Kuanzia mwaka 1885 hadi 1908, mamilioni ya watu walikufa kutokana na mauaji, mateso, njaa, na magonjwa, Idadi ya watu ilipungua kwa kiwango kikubwa katika kipindi hicho; baadhi ya waandishi wanakadiria kupoteza maisha hadi watu milioni 10[2].

  1. Read "Lost Crops of Africa: Volume III: Fruits" at nap.nationalacademies.org (kwa Kiingereza).
  2. Nzongola-Ntalaja, Georges (2002-02-01). The Congo from Leopold to Kabila: A People's History (kwa Kiingereza). Zed Books. ISBN 978-1-84277-053-5.