Nenda kwa yaliyomo

Lamia Makaddam'

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Lamia Makaddam (Kiarabu: لمياء المقدم, alizaliwa Sousse, 1971) ni mshairi, mwandishi na mtafsiri kutoka Tunisia.[1]

Lamia Makaddam alianza kuandika mashairi akiwa katika umri mdogo, na licha ya kutokuwa na waongozaji wa kike katika tasnia ya ushairi, alipata moyo na msaada kutoka kwa familia yake na walimu wake katika kazi yake ya uandishi. Shairi lake la kwanza lilichapishwa katika gazeti la mrengo wa kushoto liitwalo Badil.[2]

Ameandika vitabu viwili vya mashairi, na kazi zake zimetafsiriwa katika lugha za Kiingereza, Kifaransa, Kiholanzi na Kikurdi. Mwaka 2000, alitunukiwa Tuzo ya Fasihi ya al-Hijara nchini Uholanzi.

Ana shahada ya uzamili (MA) katika lugha na fasihi ya Kiarabu, na pamoja na kuandika, pia anafanya kazi ya utafsiri. Ameishi nchini Uholanzi kwa takribani miaka 20[2] na kwa sasa anaishi mjini Amsterdam.

  1. "بالصور.. التونسية لمياء المقدم لـ بوابة الأهرام : لا أساتذة لي في الشعر.. والمشهد مرتبك كسائر الأجناس الأدبية" [In pictures: Tunisian Lamia Makaddam to "Buwabat al-Ahram": I had no female mentors in poetry, a genre that is troubled like any other]. بوابة الأهرام (Buwaba al-Ahram) (kwa Kiarabu). 2015-11-20. Iliwekwa mnamo 2018-04-28.
  2. "Banipal (UK) Magazine of Modern Arab Literature - Contributors - Lamia Makaddam". www.banipal.co.uk. Iliwekwa mnamo 2018-04-27.
Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Lamia Makaddam' kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.