Lalla Hirayama
Mandhari
Lalla Hirayama (alizaliwa 10 Februari, 1988) ni mwigizaji, mtangazaji wa televisheni, mcheza densi na mwanamitindo kutoka nchini Afrika Kusini.
Anajulikana zaidi kwa kazi yake ya sasa kama mmoja wa watangazaji watano wa kipindi cha moja kwa moja cha habari za watu mashuhuri, V Entertainment, kinachorushwa kwenye DStv kupitia kituo cha Vuzu, ambapo ndiye mtangazaji aliyedumu kwa muda mrefu zaidi.
Pia amewahi kuwa jaji katika shindano la South Africa’s Got Talent, na ni mtangazaji wa kipindi chake binafsi kiitwacho Lalla Land kinachorushwa kwenye kituo cha M-Net Movies.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Lalla Hirayama kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |