Nenda kwa yaliyomo

Kuru (ugonjwa)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kuru (ugonjwa)
Mwainisho na taarifa za nje
Matamshi
  • IPA: kuru
Kundi MaalumuUgonjwa wa kuambukiza, nyurolojia
DaliliMitetemo, ugumu wa kutembea, maumivu ya kichwa, shida kumeza, shida ya akili, kukosa fahamu[1]
Muda wa kawaida wa kuanza kwakeMiaka 4 hadi 40 baada ya kuambukizwa[2]
VisababishiAina ya prioni[2]
Sababu za hatariUlaji wa binadamu[2]
Njia ya kuitambua hali hiiUlaji wa binadamu[2]
Utambuzi tofautiUgonjwa wa Creutzfeldt–Jakob, ukosefu wa usingizi wa kurithi unaosababisha kifo, Alzheimer, uvimbe wa ubongo, sumu ya metali nzito[2]
KingaKuepuka ulaji wa binadamu[2]
MatibabuHuduma saidizi[1]
Utabiri wa kutokea kwakeHusababisha kifo ndani ya miaka 2[2]
Idadi ya utokeaji wakeTukio la mwisho lilikuwa 2005[2] au 2009[3]
Vifo>2,700[4]

Kuru ulikuwa ugonjwa ambao ulikuwa unawaathiri Wafore na watu wa karibu wa Papua Guinea Mpya.[1][5] Dalili zake zilijumuisha kutetemeka, ugumu wa kutembea, maumivu ya kichwa, shida ya kumeza, shida ya akili, na kukosa fahamu.[1] Vicheko visivyo vya kawaida vinaweza pia kutokea.[5] Dalili zake zilizidi kuwa mbaya baada ya muda huku kifo kikitokea ndani ya miaka miwili.[1][2] Muda kati ya kuambukizwa na kuanza kwa dalili kwa ujumla ni miaka 4 hadi 40; ingawa inaweza kuwa zaidi ya miaka 50.[2]

Huenda mlipuko huu ulianza wakati mwanakijiji mmoja alipopata hali ya ghafla na wanakijiji wengine wakala ubongo wao baada ya kifo chao.[5] Kuenea kwake kuliendelea kutokana na desturi yao ya ulaji wa watu wakati wa mazishini ambapo wanafamilia waliofariki walipikwa na kuliwa.[5] Pia kuna uwezekano wa kijenetiki.[2] Utaratibu wa msingi unahusisha protini zilizokunjwa vibaya ambazo hujizalisha zenyewe na ni sugu kiasi kwamba hazivunjiki.[2] Utambuzi wake ulishukiwa kulingana na dalili na kuthibitishwa na uchunguzi wa sampuli ya tishu (biopsy) ya ubongo.[2] Ugonjwa huu ni aina ya ugonjwa wa ubongo unaoweza kuambukizwa na kuufanya ubongo kuwa na matundu kama sifongo.[2]

Kinga ni kwa kuepuka ulaji wa watu, ambao ulipungua katika maeneo yaliyoathiriwa kufuatia kupigwa kwake marufuku katika miaka ya 1950.[2][6] Usimamizi wake mzuri unahusisha huduma ya usaidizi katika juhudi za kuboresha dalili za mtu.[1] Kwa sasa, hakuna matibabu maalumu.[1]

Ugonjwa huu unaaminika kuanza karibu mwaka wa 1900 na maelezo ya kwanza ya kisayansi kutolewa mnamo 1957 na Carleton Gajdusek na Vincent Zigas.[1] Mnamo 1957, ulisababisha vifo 200 kwa mwaka, ikiwakilisha karibu 3.5% ya vifo vyote katika baadhi ya jamii.[7][5] Kwa kuwa wanawake na watoto wadogo kwa kawaida hula ubongo, waliathiriwa zaidi.[2] Kesi yake ya mwisho iliyoripotiwa ilikuwa mwaka 2005 [2] au 2009.[3] Ugonjwa huu ulikuwa ugonjwa wa kwanza wa prioni kugunduliwa.[5] Neno kúru linatokana na neno la Fore linalomaanisha "kutetemeka".[5]

  1. 1 2 3 4 5 6 7 8 Kothekar, H; Chaudhary, K (Januari 2024). "Kuru Disease: Bridging the Gap Between Prion Biology and Human Health". Cureus. 16 (1): e51708. doi:10.7759/cureus.51708. PMC 10838565. PMID 38313950.{{cite journal}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unflagged free DOI (link)
  2. 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 Mahat, S; Asuncion, RMD (Januari 2025). "Kuru". StatPearls. PMID 32644529.{{cite journal}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. 1 2 "Kuru". MRC Prion Unit and Institute of Prion diseases (kwa Kiingereza). 21 Julai 2020. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 10 Novemba 2024. Iliwekwa mnamo 2 Machi 2025.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. "Kuru: Background, Pathophysiology, Epidemiology". eMedicine. 27 Februari 2025. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 9 Oktoba 2023. Iliwekwa mnamo 2 Machi 2025.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. 1 2 3 4 5 6 7 Liberski, PP; Gajos, A; Sikorska, B; Lindenbaum, S (7 Machi 2019). "Kuru, the First Human Prion Disease". Viruses. 11 (3). doi:10.3390/v11030232. PMC 6466359. PMID 30866511.{{cite journal}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unflagged free DOI (link)
  6. Alpers, Michael P (27 Novemba 2008). "The epidemiology of kuru: monitoring the epidemic from its peak to its end". Philosophical Transactions of the Royal Society B: Biological Sciences. 363 (1510): 3707–3713. doi:10.1098/rstb.2008.0071. PMID 18849286.{{cite journal}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  7. Alpers, MP (2007). "A history of kuru". Papua and New Guinea Medical Journal. 50 (1–2): 10–9. PMID 19354007.