Kuro (jenasi)
Kuro | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Dume la kuro ndogoro
(Kobus ellipsiprymnus) | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
Spishi 6:
|
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kuro ni spishi ya kawaida zaidi ya jenasi Kobus katika familia Bovidae. Spishi nyingine za jenasi hii zinaitwa lechwe, mraye na sheshe. Kuna nususpishi mbili za kuro: (kuro) ndogoro na kuro singsing. Spishi zote zinatokea karibu na maji na hutorokea maji wakitishwa na mnyama mbua. Rangi ya spishi nyingi ni ya mchanga lakini rangi ya kuro na spishi nyingine kadhaa ni kahawia hadi kijivu au nyeusi. Mara nyingi iko rangi ya nyeupe kuzunguka macho na pua na matako. Wanyama hawa hula manyasi.
Spishi
- Kobus anselli, Lechwe wa Upemba (Upemba Lechwe)
- Kobus ellipsiprymnus, Kuro (Waterbuck)
- Kobus e. defassa, Kuro Singsing au kuro kibaka (Defassa Waterbuck)
- Kobus e. ellipsiprymnus, Kuro Ndogoro au kuro pete (Common Waterbuck)
- Kobus kob, Mraye (Kob)
- Kobus leche, Lechwe Kusi (Southern Lechwe)
- Kobus megaceros, Lechwe wa Nili (Nile Lechwe)
- Kobus vardonii, Sheshe (Puku)
Picha
-
Dume la kuro singsing
-
Jike la kuro singsing
-
Jike la kuro ndogoro
-
Dume la mraye
-
Jike la mraye
-
Madume ya lechwe kusi
-
Jike la lechwe kusi
-
Dume la lechwe wa Nili
-
Jike la lechwe wa Nili
-
Dume la sheshe
-
Jike la sheshe
Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kuro (jenasi) kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.