Kofoworola Ademola
Kofoworola Aina, Lady Ademola (Moore; 21 Mei 1913 – 15 Mei 2002) alikuwa msomi kutoka Nigeria.Alikuwa mwandishi na mtetezi wa elimu ya wanawake, na pia raisi wa National Council of Women's Societies nchini Nigeria kuanzia mwaka 1958 hadi 1964.[1]
Alikuwa mwanamke wa kwanza Mwafrika mweusi kupata shahada kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, akisoma katika St Hugh's College, na pia aliandika vitabu vya watoto.[2]
Pia alikuwa mwalimu wa kwanza mwanamke Mnigeria aliyehitimu kufundisha katika Queen’s College, mwanamke wa kwanza kuwa mwanachama na baadaye mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya United Bank for Africa, na mjumbe wa Bodi ya Udhamini wa Masomo ya Nigeria.
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Kofoworola Ademola alizaliwa tarehe 21 Mei 1913 huko Lagos. Baba yake alikuwa mwanasheria Omoba Eric Olawolu Moore, aliyekuwa wa familia ya kifalme ya Egba people|Egba. Mama yake aliitwa Aida Arabella Vaughan.
Alipata elimu katika Shule ya Wasichana ya CMS, Lagos; Vassar College nchini Marekani; na Portway College, Reading. Kuanzia mwaka 1931 hadi 1935 alisoma katika St Hugh's College, Oxford, ambapo alipata shahada ya elimu na Kiingereza.
Akiwa Oxford, aliandika wasifu mfupi kuhusu maisha yake ili kupinga mitazamo hasi ya Waingereza kuhusu Waafrika. Alieleza maisha yake kama mchanganyiko wa tamaduni za Kiafrika na Kimagharibi.
Alirejea Nigeria mwaka 1935 na kuanza kazi ya ualimu katika Queen’s College. Pia alijihusisha na mashirika ya wanawake kama YWCA.
Mwaka 1939 aliolewa na Adetokunbo Ademola. Walipata watoto watano.
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Akiwa Warri, alifundisha na kushiriki katika kikundi cha wanawake wa fasihi. Baadaye alipohamia Ibadan, alishirikiana na wanaharakati kama Elizabeth Adekogbe na Tanimowo Ogunlesi katika kuendeleza harakati za wanawake.
Mwaka 1958, alichaguliwa kuwa rais wa kwanza wa National Council of Women's Societies. Kupitia nafasi hiyo, pia alikuwa mwanachama wa Baraza la Kimataifa la Wanawake.
Alisaidia kuanzisha shule mbili: Girls Secondary Modern School, Lagos, na New Era Girls' Secondary School, Lagos.
Pia aliandika vitabu vya watoto vilivyotokana na hadithi za Afrika Magharibi, vikiwemo:
- Greedy Wife and the Magic Spoon
- Ojeje Trader and the Magic Pebbles
- Tutu and the Magic Gourds
- Tortoise and the Clever Ant
Tuzo na heshima
[hariri | hariri chanzo]Aliteuliwa kuwa Mwanachama wa Amri ya Dola ya Uingereza (MBE) mwaka 1959, akitunukiwa na Queen Elizabeth The Queen Mother. Serikali ya Nigeria pia ilimtunuku tuzo ya Order of the Federal Republic.
Pia alipokea vyeo vya kimila vya Mojibade wa Ake na Lika wa Ijemo.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Jubril Olabode Aka (2012). Nigerian Women of Distinction, Honour and Exemplary Presidential Qualities. Trafford Publishing. uk. 50.
- ↑ Pamela Roberts (2014). Black Oxford: The Untold Stories of Oxford University's Black Scholars. Andrews UK Limited.
| Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kofoworola Ademola kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |