Kleofa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kleopa)
Kleofa na mwenzake wakikutana na Yesu njiani kadiri ya mchoro wa Joseph von Führich, 1837.

Kleofa (kwa Kigiriki Κλεόπας, Kleopas[1][2][3][4][5]) alikuwa Mkristo wa karne ya 1, maarufu kwa kutokewa na Yesu Kristo mfufuka akiwa njiani kutoka Yerusalemu kwenda Emau pamoja na mwanafunzi mwingine[6] (Lk 24:13-32).

Simulizi la Injili ya Luka[hariri | hariri chanzo]

Ilikuwa siku ya tatu baada ya kifo cha Yesu, ambayo ndiyo ya ufufuko wake kadiri ya Agano Jipya. Ingawa hao wanafunzi wawili walikuwa wamesikia kwamba kaburi la Yesu lilionekana tupu, hawakupata moyo wa kubali mjini zaidi.

Njiani walikuwa wakishirikishana huzuni yao kwa Yesu kushindwa kurudisha ufalme wa Israeli. Ghafla mgeni akaongozana nao na kuulizia sababu ya huzuni yao. Baadaye aliwakaripia kwa kukosa imani akawafafanulia utabiri wa Agano la Kale kuhusu Masiya.

Walipofikia kijijini walimuomba abaki nao usiku, lakini walipoanza kula, mgeni huyo alimega mkate: ndipo walipomtambua kuwa Yesu.

Hapo mwenyewe alitoweka, nao wakarudi mjini kupasha habari kwa mitume wake, waliomuambia kwamba Yesu amemtokea pia Simoni Petro.

Habari hiyo inasimuliwa kifupi na nyiongeza ya Injili ya Marko pia (16:12-13).

Taarifa za baadaye[hariri | hariri chanzo]

Mara nyingine Kleofa huyo anasemekana ndiye yule anayetajwa na Injili ya Yohane (19:25).[7]

Mwanahistoria, askofu Eusebius wa Kaisarea, anaripoti maandishi ya Hegesippus, ambaye mwaka 180 hivi BK alisema kwamba miaka ya nyuma aliwahi kudodosa wajukuu wa Mtume Yuda akajibiwa kuwa Kleofa alikuwa ndugu wa Yosefu, mume wa Bikira Maria [8]

Tangu kale Kleofa anaheshimiwa kama mtakatifu: na Wakatoliki tarehe 25 Septemba[9], na Waorthodoksi tarehe 30 Oktoba[10], na Wakopti tarehe 10 Novemba.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Richard R. Losch All the people in the Bible: an A-Z guide to the saints 2008 Page 279 "Clopas (Κλοπας) is the Hellenized form of the Aramaic Qlopa (קלופא), while Cleopas (Κλεοπας) is a common abbreviated form of the Greek name Cleopatros (Κλεοπατρος)."
  2. St. Cleophas, Catholic Online 
  3. Apostle Cleopas, OrthodoxWiki 
  4. Joseph the Betrothed, OrthodoxWiki 
  5. An American commentary on the New Testament: Issues 13-18 Alvah Hovey - 1890 "They argue that Alphaeus is the Greek form of the Hebrew Cleophas ; that Mary, the wife of Cleophas, and the mother of James and Joses (Mark 15 ... The evidence is not entirely satisfactory that Alphaeus and Cleophas are the same name."
  6. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-02-29. Iliwekwa mnamo 2016-09-12.
  7. Tom Wright, Luke for Everyone. SPCK, London. 2002
  8. "After the martyrdom of James, it was unanimously decided that Simeon, son of Cleophas, was worthy to occupy the see of Jerusalem. He was, it is said, a cousin of the Saviour." Hegesippus noted that Cleophas was a brother of Joseph (Eusebius, Hist. eccl., III, 11).
  9. Martyrologium Romanum
  10. Cleopas, Apostle of the 70 - Online Chapel - Greek Orthodox Archdiocese of America

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kleofa kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.