Klemens Maria Hofbauer

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake iliyopo katika kaburi lake.

Klemens Maria Hofbauer (Tasovice, Moravia, leo nchini Ucheki, 26 Desemba 1751 - Vienna, Austria, 15 Machi 1820) alikuwa mtawa na padri wa shirika la Mkombozi Mtakatifu sana, ambaye anajulikana kwa kulieneza nje ya Italia na kufanya utume mkubwa sana[1].

Alijitahidi kwa namna ya ajabu kueneza imani katika nchi za mbali na kuyahuisha maisha ya Kanisa. Akiwa na akili na maadili ya hali ya juu, alivuta wanasayansi na wasanii wengi kwa Kanisa Katoliki.

Alitangazwa na Papa Leo XIII kuwa mwenye heri tarehe 29 Januari 1888, halafu Papa Pius X alimtangaza mtakatifu tarehe 20 Mei 1909.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 15 Machi[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Magnier, John. "Blessed Clement Mary Hofbauer." The Catholic Encyclopedia Vol. 4. New York: Robert Appleton Company, 1908. 27 December 2019]
  2. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.