Kindau (Bantu)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kindau ni lugha ya Kibantu nchini Msumbiji na Zimbabwe inayozungumzwa na Wandau. Isichanganywe na lugha ya Kindau izungumzwayo nchini Indonesia. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kindau nchini Msumbiji imehesabiwa kuwa watu 1,580,000. Pia kuna wasemaji 800,000 nchini Zimbabwe. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kindau iko katika kundi la S10. Kindau kinafanana sana na Kishona, na wataalamu wengine wanakiangalia kama lahaja ya Kishona tu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kindau (Bantu) kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.