Kilatini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pitio kulingana na tarehe 09:47, 17 Aprili 2015 na Baba Tabita (majadiliano | michango) (+viungo vya nje)
Systema Naturae ni kitabu maarufu kilichoandikwa manmo 1735 kwa Kilatini na Carl Linnaeus ni msingi wa uainishaji wa kisayansi wa mimea na wanyama hadi leo

Kilatini ni lugha ya kihistoria ambayo siku hizi haina tena wasemaji kama lugha ya kwanza, lakini bado hufundishwa katika shule na vyuo na hata kutumiwa kama lugha ya pili. Kilatini ilikuwa lugha hai takriban kati ya 500 KK na 600 BK na baadaye lahaja zake ziliendelea kuwa lugha za pekee zinazojulikana kama lugha za Kirumi.

Kilatini ni pia jina la mwandiko au aina ya herufi (alfabeti ya Kilatini) inayotumika kwa lugha nyingi duniani. Hata Kiswahili huandikwa siku hizi kwa herufi za Kilatini kama kwa mfano ukurasa huu wa wikipedia.

Kilikuwa

Hadi leo ni

Ramani ya uenezaji wa lugha za Kirumi za leo zilizotkana na Kilatini

Kilatini ina athira kubwa katika lugha ya sayansi na elimu. Hadi leo hufundishwa mashuleni hasa Ulaya kama lugha ya kigeni.

Kiswahili kimerithi maneno ya asili ya Kilatini hasa kupitia Kiingereza kilichopokea karibu asilimia sitini ya maneno yake yote kutoka Kilatini kupitia hasa Kifaransa. Maneno mengine ya Kilatini yameingia Kiswahili kupitia Kireno, Kifaransa n.k.

Kilatini huendelezwa na kukuzwa na wapenzi wa lugha. Kuna misamiati ya "Kilatini cha Kisasa" yenye maneno kwa ajili ya mitambo ya kisasa, mtandao n.k.. Wikipedia ya Kilatini ina makala zaidi ya 54,000.

Tazama pia

Wikipedia ya Kilatini

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kilatini kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kilatini kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.