Katherine O'Doherty
Katherine O'Doherty (3 Machi 1881 – 23 Machi 1969) alikuwa mzalendo wa Eire na mwanachama wa Cumann na mBan.[1]
Maisha ya Awali na Familia
[hariri | hariri chanzo]Katherine Gibbons alizaliwa tarehe 3 Machi 1881 huko Tyrrellspass, County Westmeath. Wazazi wake walikuwa Edward, sershenti wa Royal Irish Constabulary, na Anne Gibbons. Nyumba ya familia yao ilikuwa Collinstown, County Westmeath. Ndugu wa baba yake alikuwa kasisi na kapelani katika shule ya umma huko Yorkshire, Uingereza. Yeye ndiye aliyepanga Katherine asome huko, jambo lililomfanya awe na ufasaha katika Kijerumani.
Alisoma katika Loreto Convent, Navan kisha akajiunga katika chuo cha mafunzo ya walimu mjini Belfast. Alifundisha katika shule ya kitaifa mjini Dublin hadi mwaka 1912. Dada yake, Mother Columba wa Loreto Convent, Navan, ndiye aliyeandika wimbo wa kizalendo wa Who fears to speak of Easter week?.Mwaka 1911 aliolewa na Séamus O'Doherty.[2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Clavin, Terry (2009). "Katherine (Kitty) O'Doherty In O'Doherty, (Michael) Kevin". Katika McGuire, James; Quinn, James (whr.). Dictionary of Irish Biography. Cambridge: Cambridge University Press.
- ↑ Hughes, Paul (20 Juni 2020). "Lakeside to Stateside: the Westmeath people pushing Ireland's case in America 100 years ago". Anglo Celt. Iliwekwa mnamo 1 Oktoba 2020.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Katherine O'Doherty kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |