Karim Benzema


Karim Mostafa Benzema (alizaliwa Lyon, 19 Desemba 1987) ni mchezaji wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa. Anajulikana kama msambuliaji mwenye kipaji na mwenye nguvu.
Maisha ya klabu[hariri | hariri chanzo]
Kipindi cha awali Benzema alianza uchezaji kwenye klabu ya Terraillon akiwa na umri wa miaka 8,katika miaka ya 1990, viongozi wa Lyon walikuwa walimtembelea moja kwa moja katika swali la kumsaini kijana huyo.
Lyon Baada ya kuzungumza na babake Benzema, klabu hiyo ilimruhusu mchezaji huyo kufanyiwa majaribio na Lyon. Kufuatia majaribio hayo, Benzema alijiunga rasmi na Lyon na kuingizwa katika akademi ya klabu hiyo. Kwenye msimu wa 2004-2005 aliiwezesha timu yake kushinda makombe matatu,na msimu wa 2007-08 alibeba kombe la ligi na kuwa kombe la saba kwa Olympique Lyonnais, na kuwa mchezaji bora wa mwaka,na kuwa timu bora ya mwaka.Benzema alikuwa mfungaji bora na kushinda tuzo kutoka gazeti la Italia la Guerin Sportivo. Msimu uliofuata Olympique Lyonnais ilimuuza kwenda Real Madrid kwa ada ya £35 milioni ($50 milioni)na kusaini miaka sita. [1]
Real Madrid Baada ya kuhangaika ili aweke heshima, kwa misimu miwili alishinda magoli 32 na kuiwezesha Real Madrid kushinda Copa Del Rey mwaka 2011, na msimu wa 2011-12 alikuwa mchezaji bora mfaransa mara tatu mwaka 2011,2012,2014.[2]
Mnamo Oktoba 2021, katika kesi ya ngono ya Mathieu Valbuena, ofisi ya mwendesha mashtaka wa Versailles iliomba korti ya jinai kumpa adhabu ya kifungo cha miezi kumi kilichosimamishwa na faini ya euro 75,000.
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ "Benzema va signer Olympique Lyonnais Reserve Pro: Saison Football 2004/2005", Stat2Foot. (fr)
- ↑ Forward Benzema joins Real Madrid from Lyon. ESPN (1 July 2009).
![]() |
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Karim Benzema kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |