Kanisa kuu la Santiago de Compostela
Kanisa kuu la Santiago de Compostela ni kanisa mashuhuri lililoko Santiago de Compostela, huko Galicia nchini Hispania. Umaarufu wake umetokana kwanza na imani kwamba hapa lina kaburi la Mtakatifu Yakobo Mkubwa aliyekuwa labda mdogo wa Yesu na mmoja wa mitume wake.
Jina la Kihispania "Santiago" ni kifupi cha "Mtakatifu Yakobo" (Tiago = Yakobo).
Historia
[hariri | hariri chanzo]Mahali palianza kutambuliwa kama kaburi la mtume huyo mnamo mwaka 814. Mwaka 829 kanisa la kwanza lilijengwa hUKO[1].
Mnamo mwaka 997 kanisa hilo liliharibiwa katika mashambulio ya jeshi la Waarabu na baada ya hao kufukuzwa katika sehemu hiyo ya Hispania, kanisa lilijengwa upya miaka ya 1075 hadi 1211[2].
Jengo hilo liliendelea kuwa shabaha ya wahiji Wakristo kutoka pande zote za Ulaya.
Kanisa lilipanuliwa na kupambwa kwenye karne za 16, 17 na 18.
Jengo ni muundo wa Mtindo wa Kiroma na nyongeza za Mtindo wa Kigothi na wa Baroko baadaye.
Kanisa limepokewa na UNESCO katika orodha ya Urithi wa Dunia.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Portela Silva 2003: p. 54
- ↑ Bravo Lozano 1999: p. 235
Viungo vya Nje
[hariri | hariri chanzo]- Official website
- Reconstruction of the swinging motion of the Botafumeiro Ilihifadhiwa 23 Mei 2011 kwenye Wayback Machine.
- Photographs of the Cathedral of Santiago de Compostela, Galicia, Spain Archived 2011-02-26 at the Wayback Machine
- Pictures of Cathedral of Santiago de Compostela Ilihifadhiwa 16 Oktoba 2014 kwenye Wayback Machine.
- HyperSculpture - Pórtico de la Gloria Ilihifadhiwa 11 Februari 2015 kwenye Wayback Machine.
- The Art of medieval Spain, A.D. 500-1200, an exhibition catalog from The Metropolitan Museum of Art Libraries (fully available online as PDF), which contains material on Santiago de Compostela Cathedral (p. 175-183)
- Video clip in Youtube