Kamusi elezo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Encyclopedia Britannica ilikuwa kamusi elezo mashuhuri zaidi duniani hadi kuja kwa Wikipedia.

Kamusi elezo (pia: ensiklopedia) ni kitabu kinachojaribu kukusanya ujuzi wote wa binadamu.

Siku hizi, Wikipedia ni kamusi elezo kubwa zaidi duniani. Zamani (kabla ya kuja kwa Wikipedia) Encyclopedia Britannica ilikuwa kati ya kamusi elezo kubwa zaidi.

Katika historia zilikuwepo majaribio mbalimbali ya kukusanya ujuzi wote wa dunia. Mfano bora wa kale ni kamusi ya Yongle kutoka China iliyotungwa na wataalamu 2000 katika karne ya 14 na kuandikwa kwa mkono katika vitabu 1100.

Lakini kamusi elezo au ensiklopedia zimekuwa na athari kubwa sana tangu Johannes Gutenberg na kupatikana kwa uchapaji wa vitabu ulioshusha kabisa bei ya vitabu kwa watu wengi.

Ensiklopedia ya kwanza ya kisasa iliyokuwa na athira kubwa sana ilikuwa "Encyclopédie ou Dictionnaire raisonné des sciences, des arts et des métiers" iliyokusanywa na Denis Diderot pamoja na Jean Baptiste le Rond d’Alembert pamoja na waandishi zaidi ya 130 katika karne ya 18 huko Ufaransa. Kamusi elezo hili likawa kati ya vyanzo vya harakati ya Zama za Mwangaza.

Makala hii kuhusu kitabu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kamusi elezo kama Mwandishi wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.