Kamoya Kimeu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

'

Kamoya Kimeu
Amezaliwa1940
Kazi yakemmoja wa wavumbuzi wa mabaki ya kitambo (yaani fossil kwa Kiingereza


Kamoya Kimeu (alizaliwa mnamo 1940) ni mmoja wa wavumbuzi wa mabaki ya kitambo (yaani fossil kwa Kiingereza) waliofanikiwa sana duniani, pamoja na ushirikiano wake na wanapalantolojia Meave Leakey na Richard Leakey waliovumbua baadhi ya mabaki muhimu zaidi.

Kimeu alipata fuvu la Homo habilis lililokuwa linajulikana kama KNM ER 1813, na kiunzi karibu kamili cha Homo erectus iitwayo KNM-WT 15000 (inajulikana kama Turkana Boy au Nariokotome boy). Tena mabaki ya mamalia wawili wa aina ya "Primates" kwa lugha ya Kiingereza ambazo zinatajwa kwa jina lake: Kamoyapithecus hamiltoni na Cercopithecoides kimeui.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Kimeu alianza kazi katika paleoanthropologia kama mfanyakazi wa Louis Leakey na Mary Leakey katika miaka ya 1950.

Mwaka wa 1963 alijiunga na kundi la Richard Leakey, huku akiandamana naye hadi Mto Omo na Ziwa Rudolf (sasa Ziwa Turkana) mwaka wa 1967. Akawa kwa haraka msaidizi mkuu wa Richard Leakey, na alichukua udhibiti wa shughuli katika shamba la Leakey wakati ambao alikuwa hayupo.

Mwaka wa 1977 akawa Msimamizi wa Majumba ya Makumbusho ya Taifa la Kenya maeneo yote ya kabla ya historia nchini Kenya.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]


Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kamoya Kimeu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.