Nenda kwa yaliyomo

Juliano Cesarini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Julian Cesarini)

Juliano Cesarini (Roma, 1398Varna, Milki ya Osmani, 10 Novemba 1444) alikuwa askofu wa Frascati na mmoja wa makardinali mahiri walioteuliwa na Papa Martin V baada ya kumalizika kwa Farakano la Kanisa la Magharibi katika Kanisa Katoliki.

Uwezo wake kiakili na kidiplomasia ulimfanya kuwa mtetezi hodari wa mamlaka ya Papa dhidi ya harakati za Mtaguso wa Basel.[1]

Alianza kama mshiriki wa Mtaguso wa Basel, lakini baadaye alijitenga na harakati hiyo na kuunga mkono mamlaka kuu ya Papa. Mwandishi na askofu wa Ufaransa, Yakobo Bossuet, alimwelezea Cesarini kama ngome imara zaidi ambayo Wakatoliki waliweza kuitumia dhidi ya Wagiriki katika Mtaguso wa Firenze.[2]

  1. Cesarini genealogy, Sardimpex, ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo Mei 7, 2006, iliwekwa mnamo Januari 28, 2007{{citation}}: CS1 maint: date auto-translated (link).
  2. Miranda, Salvador. "CESARINI, seniore, Giuliano (1398-1444)". The Cardinals of the Holy Roman Church. Florida International University. OCLC 53276621. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-03-11. Iliwekwa mnamo 30 Oktoba 2021.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.