Nenda kwa yaliyomo

Joyciline Jepkosgei

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Joyciline Jepkosgei
Jepkosgei katika mbio za 2017 Prague Half Marathon
Jepkosgei katika mbio za 2017 Prague Half Marathon
Alizaliwa 8/12/1993
Nchi Kenya

Joyciline Jepkosgei (alizaliwa tarehe 8 Desemba 1993) ni mwanariadha wa mbio ndefu wa kike kutoka Kenya anayeshindana katika umbali kutoka mita 10,000 hadi marathon. Hapo awali alikuwa mshikilia rekodi ya dunia ya nusu marathon katika mashindano ya mchanganyiko wa wanaume na wanawake kwa muda wake bora wa dakika 64:51, na pia alikuwa rekodi ya dunia ya mbio za kilomita 10 kwa muda wa dakika 29:43.[1]

Mwaka 2016, alishinda medali ya shaba katika mbio za mita 10,000 kwenye Mashindano ya Afrika ya Riadha. Jepkosgei aliweka rekodi ya dunia ya nusu marathon ya saa 1:04:52 katika Prague Half Marathon mwezi Aprili 2017, na kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kuvunja muda wa dakika 65. Katika mbio hiyo, aliivunja pia rekodi zilizothibitishwa na IAAF kwa umbali wa 10 km, 15 km na 20 km, hivyo kuvunja jumla ya rekodi nne za dunia katika tukio moja. Hivyo, alikua mwanariadha wa kwanza wa Kenya kuvunja rekodi sita za dunia ndani ya miezi sita.[2]

  1. Kelsall, Christopher (2019-02-14). "World record holder Joyciline Jepkosgei runs marathon debut in Hamburg". Athletics Illustrated (kwa Canadian English). Iliwekwa mnamo 2019-02-14.
  2. Joyciline Chepkosgei. Association_of_Road_Racing_Statisticians. Retrieved on 1 April 2017.
Makala hii kuhusu mwanariadha wa Kenya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Joyciline Jepkosgei kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.