Jimbo Katoliki la Morogoro

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Jimbo la Morogoro (kwa Kilatini: Dioecesis Morogoroensis) ni mojawapo katika ya majimbo 35 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania kwa ajili ya waumini wake katika manispaa ya Morogoro pamoja na wilaya za Bagamoyo, Morogoro vijijini, Mvomero, Kilosa, Gairo n.k.

Eneo lote lina kilometa mraba 43,380.

Kutokana na historia yake linafuata mapokeo ya Kanisa la Kiroma, kama majimbo mengine yote ya Tanzania.

Historia yake[hariri | hariri chanzo]

  • 11 Mei 1906: Kuundwa kama Apostolic Vicariate of Central Zanguebar kutokana na Apostolic Vicariate of Zanzibar
  • 21 Desemba 1906: Kubadilishiwa jina kuwa Apostolic Vicariate of Bagamoyo
  • 25 Machi 1953: Kupandishwa hadhi kuwa Diocese of Morogoro

Uongozi wake[hariri | hariri chanzo]

Papa analisimamia jimbo pia kupitia Idara ya Uinjilishaji wa Mataifa.

Kazi zake[hariri | hariri chanzo]

Likiishi katika eneo ambapo wananchi walio wengi ni Waislamu, linajadiliana nao kwa amani pamoja na kutangaza Injili ya Yesu Kristo.

Likitegemea uwezo wa Roho Mtakatifu katika liturujia linazidi kuwatakasa watu ili waishi kama watoto halisi wa Baba wa mbinguni.

Kwa mamlaka waliyokabidhiwa kwanza Mitume wa Yesu na kurithiwa kwa sakramenti ya daraja, linazidi kuwachunga waamini washuhudie upendo kati yao na kwa wote, hasa kwa kutumikia wanaohitaji huduma zake mbalimbali za kijamii pia (upande wa afya, elimu, n.k.).

Miundo na michango ya waamini mbalimbali[hariri | hariri chanzo]

Mbali ya ofisi na taasisi mbalimbali (k.mf. seminari), miundo yake ya msingi ni parokia zilizoenea katika wilaya zake zote na zinazoongozwa na mapadri wanajimbo na wanashirika, ambao baadhi yao ni wazawa, baadhi walitokea nchi za jirani na za mbali (hasa Asia na Ulaya).

Watawa wa kike na wa kiume wengi wa mashirika 40 hivi wanatoa mchango wa pekee kwa kushuhudia maisha ya Yesu katika useja mtakatifu, ufukara na utiifu.

Hatimaye walei, ambao ndio wanakanisa walio wengi, wanatimiza utume wao katika majukumu ya kila siku ya maisha ya kawaida vijijini na mitaani, wakishirikiana katika mtandao wa vigango, vinavyotegemea sana makatekista, na wa jumuia ndogondogo za Kikristo, zilizopewa kipaumbele na Sinodi ya Afrika.

Malengo[hariri | hariri chanzo]

Ni juhudi yao kulenga hali ya kujitegemea hata kiuchumi, ingawa hali halisi ya nchi ni ngumu kwa sababu zilezile zilizoathiri karibu nchi zote za bara hilo.

Wakitegemea neema ya Mungu, ni juhudi yao hasa kushinda dhambi ndani mwao wenyewe na ndani ya miundo ya jamii ili utawala wa Mungu uenee kote na kuleta utakatifu na wokovu, haki na amani.

Takwimu[hariri | hariri chanzo]

Mwishoni mwa mwaka 2021 jimbo lilikuwa na waamini waliobatizwa 778,100 kati ya wakazi 1,838,700 (42.3%).

Katika parokia 63 kulikuwa na mapadri 179 (wanajimbo 86 na watawa 93), mabradha na mafrateri watawa 444 na masista 691.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Kuanzia tarehe 13 Februari 2019 mamlaka yote jimboni imekabidhiwa na Papa Fransisko kwa Msimamizi wa Kitume padri Lazarus Vitalis Msimbe, SDS.
  2. "Rinunce e nomine, 13.02.2019". Vatican.va. Iliwekwa mnamo 13 February 2019.  Check date values in: |accessdate= (help)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jimbo Katoliki la Morogoro kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.