Jimbo Katoliki la Kapsabet
Mandhari
Jimbo Katoliki la Kapsabet ni mojawapo kati ya majimbo 28 ya Kanisa Katoliki nchini Kenya. Lipo chini ya jimbo kuu la Kisumu. Makao makuu yako Kapsabet.
Tarehe 10 Julai 2025 limeanzishwa kwa kumega Jimbo Katoliki la Eldoret upande wa kaunti ya Nandi. Kama Askofu wake wa kwanza ameteuliwa John Kiplimo Lelei.
Jimbo jipya lina Km2 2,888.4, wanapoishi watu 885,711, ambao kati yao Wakatoliki ni 313,655.
Parokia ni 36, mapadri ni 52, wakiwemo wanajimbo 44, watawa wa kike ni 44, waseminari ni 29 na makatekista 316.
| Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Jimbo Katoliki la Kapsabet kama historia yake au maelezo zaidi? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |