Nenda kwa yaliyomo

Janja

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Janja
Janja kungu (Lutjanus bohar)
Janja kungu (Lutjanus bohar)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Actinopterygii (Samaki walio na mapezi yenye tindi)
Oda: Acanthuriformes (Samaki kama janja)
Familia: Lutjanidae (Samaki wanaofanana na janja)
Gill, 1861
Jenasi: Lutjanus
Bloch, 1790
Ngazi za chini

Spishi 73, 18 katika Afrika ya Mashariki:

Janja ni samaki wa baharini wa jenasi Lutjanus katika familia Lutjanidae ya oda Acanthuriformes katika ngeli Actinopterygii walio maarufu kwa matumizi. Majina mengine yatumikayo kwa spishi kadhaa ni tembo na kungu, lakini hayo hutumika pia kwa spishi za jenasi na familia nyingine. Wanatokea kwa kawaida katika maji ya kitropiki na kinusutropiki ya Bahari za Atlantiki, Hindi na Pasifiki kwenye miamba ya matumbawe na kapa. Spishi kadhaa wanatokea maji matamu au chumvi kidogo.

Jenasi hii ina spishi 73 duniani kote. Spishi 18 zimeriportiwa kutoka Afrika ya Mashariki.

Spishi za Afrika ya Mashariki

[hariri | hariri chanzo]