Nenda kwa yaliyomo

Janice Boddy

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Janice Boddy ni mwanaanthropolojia kutoka Kanada. Kama Profesa wa Anthropology katika Chuo Kikuu cha Toronto,[1] Boddy anajitolea katika anthropolojia ya matibabu, dini, masuala ya jinsia, na ukoloni katika Sudan na Mashariki ya Kati. Yeye ni mwandishi au mwandishi mwenza wa vitabu Wombs and Alien Spirits (1990), Aman: The Story of a Somali Girl (1995), na Civilizing Women: British Crusades in Colonial Sudan (2007).

Katika makala yake "Womb as oasis: the symbolic context of Pharaonic circumcision in rural Northern Sudan" (American Ethnologist, 1982), Boddy alielezea wazo la kuweka katika muktadha wa kitamaduni ukeketaji wa wanawake Afrika kwa wale wanaotaka kuona tamaduni hii ikikemewa na kuachwa.

Boddy alipata Shahada ya Kwanza (BA) kutoka Chuo Kikuu cha McGill, Shahada ya Uzamili (MA) kutoka Chuo Kikuu cha Calgary na, mwaka 1982, alipata PhD kutoka Chuo Kikuu cha British Columbia

Inadhaniwa kwamba Boddy alikuwa mwanamke wa kwanza kutoka Chuo Kikuu cha Toronto Scarborough kuchaguliwa katika Jumuiya ya Kifalme ya Kanada. Mwanamke wa pili, Lisa Jeffrey, alichaguliwa mwaka 2007.[2]

  1. "Janice Boddy | Anthropology". anthropology.utoronto.ca (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2026-01-18.
  2. "Mathematics professor at U of T Scarborough named to Royal Society | University of Toronto Scarborough News". utsc.utoronto.ca (kwa Kiingereza). 2007-07-27. Iliwekwa mnamo 2026-01-18.