Nenda kwa yaliyomo

James Wapakhabulo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

James Francis Wambogo Wapakhabulo (23 Machi 194527 Machi 2004) alikuwa mwanasiasa wa Uganda ambaye alihudumu kama Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda kuanzia mwaka 2001 hadi 2004.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Wapakhabulo alianza kazi yake kwa kusoma sheria katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki (sasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam). Kuanzia miaka ya 1960 hadi kuanguka kwake mwaka 1977, alifanya kazi kama katibu na mtafsiri wa kisheria katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Baada ya hapo mwaka huo, alihamia Papua New Guinea akiwa mwanatafsiri wa kisheria wa ngazi ya juu na baadaye afisa mkuu wa kisheria. Aliendelea na kazi hiyo hadi mwaka 1986.

Kazi ya kisiasa

[hariri | hariri chanzo]

Wapakhabulo alihusishwa na chama kilichokuwa madarakani cha National Resistance Movemen. Baadaye aligombea Ubunge, na kati ya 1994 na 1995 alikuwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba. Mwaka 1996, alipewa nafasi ya Spika wa Bunge, nafasi aliyoishikilia hadi 1998. Mwaka 1998, aliteuliwa kama Kamishna wa Siasa wa Taifa katika mfumo wa kisiasa wa Uganda wa bila vyama hadi mwaka 2001 alipokuwa Naibu Waziri Mkuu wa Pili na Waziri wa Mambo ya Nje. Alishikilia nafasi zote mbili hadi kifo chake.[1][2]

  1. Bryant, Nick (11 Juni 2014). "Uganda's Sam Kutesa Elected As UN General Assembly President". BBC News. Iliwekwa mnamo 20 Machi 2015.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. Speakers of Parliament In Uganda Since 1962 Archived 2017-10-29 at the Wayback Machine
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu James Wapakhabulo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.