Isobel Forrester
Isobel Forrester (jina la kuzaliwa: Isobel Margaret Stewart McColl; 1895 - 1976) alikuwa mshiriki wa madhehebu ya kiekumeni aliyezaliwa Uskoti. Alikuwa mwenyekiti na mwanachama hai wa Chama cha Makanisa ya Kiekumeni cha Uskoti.
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Forrester alizaliwa katika jumba la kifahari huko Glenlyon. Alikuwa mzaliwa wa kwanza kwa Jane Mary (Jeannie) (aliyezaliwa Baillie) na John McColl. Sir Walter Scott alielezea Glenlyon kama "bonde refu zaidi, lenye upweke na kupendeza zaidi huko Uskoti".[1] Familia yake ililazimika kuondoka katika jumba hilo mwaka 1904, kwa sababu ya migogoro katika kanisa la baba yake.[2]
Alikuwa mwenyekiti na mwanachama hai wa Chama cha Kiekumeni cha Makanisa ya Uskoti.[2] Alikuwa mfuasi mwenye shauku wa kuwekwa wakfu kwa wanawake kuwa mchungaji.[3] Idhini ilipotolewa kwa wanawake kuwekwa wakfu, alimtumia mke wake telegramu, Margaret Forrester nchini India akimwambia kuhusu "ushindi mkubwa" mnamo Mei 1968.[4] Margaret aliwekwa wakfu[5] na baadae akawa mwandishi wa watoto.[6]
Alifariki huko York mnamo Agosti 1976 na mazishi Pamoja na uchomaji wa mwili wake vilifanyika Edinburgh mnamo Septemba 1976.[2] Nyaraka zinazohusiana na kitabu chake na mawasiliano ziko katika Chuo Kikuu cha Edinburgh.[7]
Maisha binafsi
[hariri | hariri chanzo]Aliolewa na William Forrester ambaye alikuwa mwanatheolojia. Mtoto wao wa mwisho kati ya watoto watano[8] alikuwa Duncan Baillie Forrester. Alizaliwa mwaka 1933 na baadae akawa profesa wa theolojia katika Chuo Kikuu cha Edinburgh.[9]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://books.google.co.tz/books?id=gChVDwAAQBAJ&pg=PA20&redir_esc=y
- 1 2 3 https://www.oxforddnb.com/display/10.1093/ref:odnb/9780198614128.001.0001/odnb-9780198614128-e-66407
- ↑ https://silo.pub/biographical-dictionary-of-scottish-women.html
- ↑ https://silo.pub/biographical-dictionary-of-scottish-women.html
- ↑ https://books.google.co.tz/books?id=xBCH2wXyjmsC&dq=%22isobel+forrester%22&pg=PA77&redir_esc=y#v=onepage&q=%22isobel%20forrester%22&f=false
- ↑ https://books.google.co.tz/books?id=IAR3MAEACAAJ&redir_esc=y
- ↑ https://archives.collections.ed.ac.uk/agents/people/1712
- ↑ https://www.scotsman.com/news/obituaries-duncan-forrester-1460501
- ↑ https://www.encyclopedia.com/arts/educational-magazines/forrester-duncan-b-1933
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |