Shoro (Hyliidae)
Mandhari
(Elekezwa kutoka Hylia)
| Shoro | ||||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
| Ngazi za chini | ||||||||||||||
|
Jenasi 7, spishi 2 katika Afrika:
|
Shoro wa familia Hyliidae katika familia ya juu Sylvioidea ni spishi mbili za ndege wadogo wanaotokea Afrika kusini mwa Sahara. Kwa sababu wanafanana kila mmoja sana lakini kutofautiana na shoro wa familia nyingine, wanaainishwa katika familia yao yenyewe.
Kwa kawaida hupatikana katika matabaka ya chini ya kanopi ya misitu ya mvua ya kitropiki. Hujenga kiota cha mviringo au chenye umbo la duaradufu chenye mlango wa pembeni (kwa mwisho wa mlizamu katika Pholidornis) kutokana na mabaki ya mimea yaliyolegea yaliyoshikiliwa pamoja na nyuzi za mimea. Jike hutaga yai moja au mawili meupe. Wanaweza kuonyesha uzalizaji wa ushirika.
Spishi
[hariri | hariri chanzo]- Hylia prasina, Shoro kijani (Green hylia)
- Pholidornis rushiae, Shoro mdogo (Tit hylia)
Picha
[hariri | hariri chanzo]- Shoro mdogo