Nenda kwa yaliyomo

Shoro (Hyliidae)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Hylia)
Shoro
Shoro kijani
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Sylvioidea (Ndege kama kucha)
Familia: Hyliidae (Ndege walio na mnasaba na kuchanyika)
Bannerman, 1923
Ngazi za chini

Jenasi 7, spishi 2 katika Afrika:

Shoro wa familia Hyliidae katika familia ya juu Sylvioidea ni spishi mbili za ndege wadogo wanaotokea Afrika kusini mwa Sahara. Kwa sababu wanafanana kila mmoja sana lakini kutofautiana na shoro wa familia nyingine, wanaainishwa katika familia yao yenyewe.

Kwa kawaida hupatikana katika matabaka ya chini ya kanopi ya misitu ya mvua ya kitropiki. Hujenga kiota cha mviringo au chenye umbo la duaradufu chenye mlango wa pembeni (kwa mwisho wa mlizamu katika Pholidornis) kutokana na mabaki ya mimea yaliyolegea yaliyoshikiliwa pamoja na nyuzi za mimea. Jike hutaga yai moja au mawili meupe. Wanaweza kuonyesha uzalizaji wa ushirika.