Hifadhi ya Taifa ya Mudumu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Hifadhi ya Taifa ya Mudumu
Hifadhi ya Taifa ya Mudumu

Hifadhi ya Taifa ya Mudumu, ni hifadhi ya taifa katika Mkoa wa Caprivi kaskazini mashariki mwa Namibia . Hifadhi hiyo ilianzishwa mnamo 1990. Inachukua eneo la kilomita za mraba 737. Mto Kwando unaunda mpaka wa magharibi na Botswana . Hifadhi mbalimbali za maeneo ya jumuiya na misitu ya jamii yanazungukwa na hifadhi ya taifa ya Mudumu. [1]

Eneo hili ni njia muhimu ya uhamiaji kutoka Botswana hadi Angola kwa wanyama wakubwa kama vile tembo wa Kiafrika . [2] [3]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mbuga ya taifa ya Mudumu ilianzishwa mwaka 1990, muda mfupi kabla ya uhuru wa Namibia . [4] Ingawa saizi iliyoidhinishwa ya mbuga hiyo ni kilomita za mraba 1,010, ila ukubwa halisi ni kilomita za mraba 737. [5]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. State of Protected Areas in Namibia. Windhoek, Namibia: Ministry of Environment and Tourism, Namibia. 2010. p. 172. 
  2. . Windhoek, Namibia: Ministry of Environment and Tourism. 2009. p. 4.  Missing or empty |title= (help)
  3. Draft management plan for Mudumu National Park. Windhoek, Namibia: Ministry of Environment and Tourism. 2012. p. 58. 
  4. . Windhoek, Namibia: Ministry of Environment and Tourism. 2009. p. 4.  Missing or empty |title= (help)
  5. State of Protected Areas in Namibia. Windhoek, Namibia: Ministry of Environment and Tourism, Namibia. 2010. p. 172.