Hifadhi ya Comoé

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Comoé National Park

Ramani ya mto Comoe katika Cote d'Ivoire, hifadhi iko kaskazini kabisa
MahaliCôte d'Ivoire
Eneokm2 11 500 (sq mi 4 400)
Kuanzishwa1983

Hifadhi ya Comoé ni hifadhi ya bioanwai iliyoandikishwa katika orodha ya UNESCO ya Urithi wa Dunia nchini Cote d'Ivoire. Ni hifadhi kubwa zaidi inayolindwa huko Afrika Magharibi, ikiwa na eneo la km2 11,500. Upande wa kusini inaanza katika sehemu yenye mchanganyiko wa savana na misitu ikiendelea hadi maeneo yabisi ya kaskazini.[1]

Kando ya Mto Comoé kuna bado sehemu za misitu ya mvua ya kitropiki ambayo kawaida hupatikana kusini tu. [2]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mazingira ya hifadhi ya Comoé yalikuwa na wakazi wachache tangu kale kutokana na ardhi isiyo na rutuba, kupatikana kwa upofu wa mto kwenye mito na wingi wa mbu wa mbung'o wanaoeneza ugonjwa wa malale pamoja na nagana ya mifugo[3][4].

Wakoloni Wafaransa walitenga maeneo baina ya mito Comoe na Boua kuwa hifadhi ya wanyama. Hifadhi hiyo ilipanuliwa baada ya uhuru.

Mto Comoe unapitia mbuga.
Savana katika Hifadhi ya Kitaifa ya Comoé.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Hifadhi hiyo inafanywa hasa na tambarare zilizopitiwa na Mto Comoé pamoja na matawimito yake (mto Iringou, mto Bavé, mto Kongo).

Kuna pia madimbwi mbalimbali ya kudumu pamoja na mengine yanayokauka wakati wa kiangazi.

Ardhi ni kwa sehemu kubwa duni na haifai kwa kilimo. Milima midogo kadhaa inainuka hadi mita 600 juu ya uwiano wa eneo ambalo kwa kawaidi liko mita 120-500 juu ya usawa wa bahari.[1]


Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 Konaté, Souleymane; Kampmann, Dorothea (2010). Biodiversity Atlas of West Africa, Volume III: Côte d'Ivoire. Abidjan & Frankfurt/Main: BIOTA. ISBN 978-3-9813933-2-3. 
  2. "Wildlife authority of Côte d’Ivoire awarded Rapid Response Facility grant to combat poaching after period of civil unrest". UNESCO. Iliwekwa mnamo 4 August 2015.  Check date values in: |accessdate= (help)
  3. Kronberg, FGU (September 1979). Gegenwärtiger Status der Comoé und Tai Nationalparks sowie des Azagny-Reservats und Vorschläge zu deren Erhaltung und Entwicklung zur Förderung des Tourismus. Eschborn: Deutsche Gesellschaft für Teschnische Zusammenarbeit (GTZ). ku. 12–13.  Check date values in: |date= (help)
  4. Cormier-Salem, Marie-Christine; Juhé-Beaulaton, Dominique; Boutrais, Jean; Roussel, Bernard (2005). Patrimoines naturels au Sud : territoires, identités et stratégies locales. Paris: IRD éditions. ISBN 2-7099-1560-X. 
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hifadhi ya Comoé kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.